WACHIMBAJI WADOGO SHINYANGA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU MFUMO MPYA WA UTOAJI LESENI ZA MADINI KWA NJIA YA MTANDAO

 Kamishna Msaidizi wa Madini, Kanda ya Kati – Magharibi, Humphrey Mmbando akitoa ufafanuzi wa baadhi ya masuala muhimu yaliyojitokeza wakati wa semina kwa wachimbaji wadogo wa madini kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji wa leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Semina hiyo imefanyika leo mjini Shinyanga na ni mwendelezo wa Mafunzo yanayotolewa nchi nzima kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini. Wengine pichani (mstari wa mbele) ni baadhi ya Maofisa kutoka Ofisi ya Madini – Shinyanga.
 Baadhi ya akina mama ambao ni wachimbaji wadogo wa madini mkoani Shinyanga wakiwa katika semina kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Kutoka Kushoto ni Amina Mtoro, Hafsa Issa, Halima Mohamed, Khadija Salum na Nusura Juma. Semina hiyo imefanyika leo mjini Shinyanga na ni mwendelezo wa Mafunzo yanayotolewa na Wizara ya Nishati na Madini kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchi nzima.
 Mtaalamu kutoka Kitengo cha Leseni cha Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Nuru Shabani, akitoa ufafanuzi kuhusu utaratibu wa utoaji wa leseni kwa njia ya mtandao wakati akiwasilisha mada kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP) kwa wachimbaji madini wadogo, wakati wa Semina maalumu iliyofanyika leo Septemba 9, 2015 mjini Shinyanga.
 Mtaalamu kutoka Kitengo cha Leseni, Wizara ya Nishati na Madini, Juma Masoud akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa wakati wa Semina kwa wachimbaji wadogo wa madini kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Semina hiyo imefanyika leo Septemba 9, 2015 mjini Shinyanga ikiwa ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa na Wizara husika kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini kote.
 Baadhi ya Vijana ambao ni wamiliki wa leseni za madini mkoani Shinyanga wakiwa katika Semina kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining cadaster Transactional Portal – OMCTP) yanayotolewa na Wizara ya Nishati na Madini nchi nzima. Kutoka Kushoto ni Juma Swalehe, Steven Ngonyani, Salum Abdillah na Meshack Daniel. Mafunzo hayo kwa mkoa wa Shinyanga, yamefanyika leo Septemba 9, 2015.
Mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Erick Mkoma, akisaini Kitabu cha Wageni katika Ofisi ya Madini Kanda ya kati Magharibi iliyoko mjini Shinyanga. Wengine pichani ni Juma Masoud (katikati) na Mhandisi Nuru Shabani (Kulia). Wataalam hawa leo Septemba 9, 2015 wametoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini mkoani Shinyanga kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandano (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP).

Na Veronica Simba – Shinyanga
Zoezi la utoaji semina kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini linaloendeshwa na wizara ya nishati na madini leo limefanyika mjini Shinyanga ambapo wachimbaji zaidi ya 60 wamepatiwa mafunzo hayo.
Akifungua Semina hiyo mjini Shinyanga, Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kati Magharibi, Humphrey Mmbando amewataka washiriki kuhakikisha wanaufahamu mfumo mpya wa utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP) kwani ni wale tu watakaosajiliwa kwenye mfumo husika ndiyo watakaotambuliwa kisheria na kupata haki zote za msingi.
Wizara ya Nishati na Madini ilizindua mfumo wa kutoa huduma za leseni kwa njia ya mtandao mapema mwezi Juni mwaka huu mjini Dodoma ili kutoa huduma za haraka, kuongeza uwazi na kumuwezesha mteja kusimamia leseni zake mwenyewe.
Ni kwa kuzingatia umuhimu wa matumizi ya mfumo huo mpya kwa wadau wa sekta ya madini nchini, Wizara kupitia Kitengo cha Usimamizi wa Leseni inaendesha zoezi nchi nzima kuwaelimisha wadau hao namna mfumo huo unavyofanya kazi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni