Kamishina
 wa Elimu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Eusella 
Bhalalusesa akizungumza kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu Wizara ya 
Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome kuzindua maonesho ya 
Tehama yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwl. 
Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Na mwandishi wetu
JUMLA
 ya wanafunzi 60,000 katika shule 150 nchini wamepitiwa na mafunzo ya 
programu ya Bridge IT yenye lengo la kuongeza ubora wa elimu kwa kutumia
 teknolojia ya kisasa ya kidijiti (digital technology) katika 
ufundishaji na ujifunzaji wa Hisabati,Sayansi na Stadi za Maisha.
Hayo
 yamsemwa na Kamishina wa Elimu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, 
Profesa Eusella Bhalalusesa akimkaribisha Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na
 Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome kuzindua maonesho ya Tehama.
Alisema
 kutokana na mafanikio yaliyotokea sasa wanatanua wigo baada ya 
kuwezeshwa kifedha na Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya elimu (Global
 Partnership For Education) kwa ajili ya kuendeleza teknolojia hiyo 
katika kujifunza na kufundisha katika shule za msingi na hasa darasa la 
awali la kwanza hadi la nne.
Aidha
 maonesho hayo yanayofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu 
Julius Nyerere yana lengo la kuonesha ubunifu ambao upo tayari kutumika 
kufanikisha mafunzo hayo.
Pia
 maonesho hayo yanatarajia kujadili na kuangalia mbinu za kielektroniki 
zitakazoweza kuendana na mazingira ya Tanzania katika ufundishaji na 
kujifunza kwa gharama nafuu.
Pia wanatarajia kuangalia utayari wa walimu na namna ya kuwabadilisha mtazamo ili waweze kufundisha na kufundishika.
“Lengo
 la serikali kupitia Wizara ya Elimu ni kupanua wigo wa elimu hasa elimu
 ya awali kwa kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano ambayo 
itabadilisha ufundishaji kutoka kutumia vitabu vilivyopo katika mfumo wa
 ‘hard copy’ na kuwa katika mfumo wa sauti na picha au ‘soft copy’,” 
alisema Profesa Bhalalusesa.
Katibu
 Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome 
akifuatilia kwa makini risala Kamishina wa Elimu Wizara ya Elimu na 
Mafunzo ya Ufundi, Profesa Eusella Bhalalusesa (hayupo pichani).
Alisema
 hadi kufikia wakati huu serikali imeshapiga hatua kubwa katika matumizi
 ya Tehama ambayo katika majaribio yake yameonesha kufanikiwa na wadau 
mbalimbali wa elimu wameyapongeza na kuyaunga mkono.
Profesa
 Bhalalusesa alisema kwa sasa wagunduzi mbalimbali wa mifumo ya Kompyuta
 inayoweza kutumika kufundishia ndio watakoonesha kazi zao na kutoa 
ufafanuzi wa kina kwa majaji wataochagua kazi chache na kuzifanyia 
majaribio kabla ya kuanza kutumika kufundishia.
Kwa
 Upande wake Mratibu wa Mpango wa Kukuza stadi za Kusoma, Kuandika na 
Kuhesabu kutoka Wizara ya Elimu, Agripina Habichi alisema mpango huo wa 
matumizi ya Tehama utasaidia wanafunzi kufahamu kusoma na kuandika kabla
 ya kuendelea na masomo ya darasa la tatu.
“Maonesho
 haya yanafanyika katika wakati muafaka ukizingatia tunataka kupiga 
hatua kubwa katika kuboresha elimu yetu. Washiriki wa maonesho haya 
wamekuja kutuonesha utawaalamu wao unaoweza kutumika kufundishia.
Lengo
 letu ni kuwafikia wanafunzi wengi zaidi ambapo tumeazimia kuzifikia 
shule zaidi ya 2000 katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 na hivyo tutakuwa
 katika kiwango bora zaidi cha utoaji wa elimu inayojitosheleza,” 
alisema Habichi.
Katibu
 Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome 
akizungumza kabla ya kuzindua rasmi maonesho ya Tehama yanayoendelea 
katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar
 es Salaam.
Katika
 maonesho hayo serikali imesema inatarajia kuanza kutumia rasmi 
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) katika kufundishia 
wanafunzi kuanzia ngazi ya chini kabisa ya elimu ambayo ni chekechea.
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome 
alisema matumizi ya Tehama katika ufundishaji wa wanafunzi wa chekechea 
yataimarisha kiwango cha elimu.
“Dunia
 imebadilika sana hasa katika sekta ya elimu na mawasiliano, hatuna budi
 kuendana nayo kwa kasi ileile ya ukuaji wake kwa kuimarisha mifumo yetu
 ya ufundishaji,” alisema Profesa Mchome.
Alisema
 wizara yake imeanzisha mpango maalum utakaosaidia wanafunzi kujifunza 
kwa njia ya kisasa ya kutumia mbinu za kielektroniki katika kujifunza na
 hivyo kuimarisha uelewa na kuongeza hamasa ya ufundishaji kwa 
wanafunzi.
Profesa
 Mchome alisema maonesho hayo yana lengo la kupata wadau mbalimbali 
waliobuni programu zinazoweza kutumika katika kufundishia kwa kutumia 
mifumo ya kielektroniki na hivyo watachaguliwa wachache wenye sifa na 
watakowezesha mafunzo hayo katika shule za Msingi na baadae katika ngazi
 ya sekondari.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome akijianda kuzindua rasmi maonesho ya Tehama yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Sasa yamezinduliwa rasmi.
Ofisa
 Miradi ya Elimu kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na
 Utamaduni (UNESCO), Faith Shayo akitoa maelezo ya shughuli mbalimbali 
zinazofanywa na shirika lake katika kuendeleza sekta ya elimu nchini kwa
 Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome 
(kushoto) mara baada ya kuzindua maonesho hayo ambapo pia UNESCO 
inashiriki. Katikati ni Kamishina wa Elimu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
 Ufundi, Profesa Eusella Bhalalusesa.
Ofisa
 anayeshughulikia masuala ya Elimu Kitaifa wa UNESCO, Tumsifu Mmari 
(katikati) akimsikiliza mmoja wa wadau wa elimu aliyetembelea banda la 
UNESCO kwenye maonesho ya TEHAMA yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano
 wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Kushoto ni 
Ofisa Miradi ya Elimu kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, 
Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Faith Shayo.
Ofisa
 anayeshughulikia masuala ya Elimu Kitaifa wa UNESCO, Tumsifu Mmari 
(kulia) akiwa na wadau wengine wa elimu wakipitia makbrasha mbalimbali 
katika mkutano huo.
Pichani juu na chini ni baadhi wadau wa elimu waliohudhuria uzinduzi wa maonyesho hayo.
Baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali za msingi jijini Dar walioshiriki hafla hiyo.
Mkurugenzi
 Mkuu wa Shule Direct, Faraja Nyalandu akipozi na wadau kwenye ukumbi wa
 mikutano wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es Salaam 
yanakoendelea maonesho ya TEHAMA.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni