TOTTENHAM, SCHALKE NA BORUSSIA DORTMUND WAANZA KWA USHINDI LIGI YA UROPA

Michuano ya Ligi ya Uropa imeanza rasmi kwa msimu wa 2015-2016 huku ikishudia timu za Tottenham, Schalke na Borussia Dortmund wakianza kwa ushindi.

Tottenham wakiwa nyumbani kwenye dimba la White Hart Lane waliibuka na ushindi wa mabao 3 -1 dhidi ya FK Qarabag, ambapo Heung-min Son alicheka na nyavu mara mbili.
                                                      Heung-min Son akishangilia moja ya bao lake 
Apoel Nicosia wakiwa wenyeji wa Schalke walikubali kichapo cha mabao 3-0, huku Borussia Dortmund wakishinda kwa mabao 2-1 dhidi ya FK Krasnodar.

Matokeo mengine ya michuano hiyo ni Ajax 2-2 Celtic, Bordeaux 1-1 Liverpool
Fenerbahçe 1-3 Molde na Anderlecht 1-1 Monaco.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni