KIFO CHA MFANYAKAZI WA IKULU CHAMHUZUNISHA RAIS BARACK OBAMA

Rais Barack Obama wa Marekani amesema kuwa amevunjika moyo baada ya mfanyakazi mmoja mwandamizi wa Ikulu kufa katika ajali ya baiskeli wakati wa shuguli ya kujitolea.

Mfanyakazi huyo Jake Brewer, 34, alikufa wakati akishiriki msafara wa baiskeli wa kukabiliana na Saratani siku ya jumamosi.

Afisa huyo ushauri wa sera katika ofisi ya mkuu wa teknolojia alishindwa kumudu baiskeli yake na kugongwa na gari.

Rais Obama amesema marehemu Jake alijitolea maisha yake katika kuwawezesha watu, na kuifanya serikali kufanya kazi vyema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni