Na John Gagarini, Lugoba 
 Wagombea
 wa nafasi za uongozi hapa nchini wametakiwa kukubali matokeo mara 
uchaguzi utakapofanyika Oktoba 25 mwaka huu kwani kuna maisha mengine 
baada ya uchaguzi, na   kuendelea kufanya kampeni zao huku wakiendelea 
kuhubiri na kulinda amani iliyopo kwani wana nafasi kubwa ya 
kuwashawishi wafuasi wao wasifanye vurugu au kufanya vitendo 
vinavyosababisha uvunjifu wa amani. 
 Pia
 wagombea watakaoshindwa kwenye uchaguzi mkuu wameombwa wakubali matokeo
 kwani kwenye washindani lazima kuwe na washindwa ili kuondoa hali ya 
mafarakano kwani kwa wale watakaoshindwa wasipokubali matokeo wanaweza 
kuleta uvunjifu wa amani. 
 Hayo
 yalisemwa katika  Kijiji cha Maviayangombe kata ya Lugoba wilayani 
Bagamoyo mkoani 
Pwani na Askofu mkuu wa Dayosisi ya Morogoro ya Kanisa la Kiinjili la 
Kilutheri Tanzania (KKKT) Jacob Mameo Ole Paulo wa Dayosisi ya Morogoro 
wakati wa mazishi ya mtoto wa aliyekuwa kiongozi wa wafugaji Laban 
Moreto, Karokya Moreto (33) ambaye alikuwa mwanajeshi wa kikosi cha 
04/691 cha Mtwara. 
 Askofu
 Ole Paulo alisema kuwa wagombea hao wanauwezo wa kudumisha amani kwa 
kuhubiri au kuingiza nchi kwenye machafuko endapo watayatumia vibaya 
majukwaa wakati wa kipindi hichi cha kampeni za uchaguzi. 
 “Wanapaswa
 kuhubiri amani na kuacha kutumia maneno yatakayo haribu amani ya nchi 
iliyopo ambayo imedumu kwa kipindi kirefu tangu nchi ilipopata uhuru 
miaka zaidi ya 50 hivyo itakuwa ajabu ivunjwe kisa kuwania uongozi tu,” 
alisema Askofu Ole Paulo. 
Alisisitiza
 kuwa vyama vya siasa vinapaswa kupingana kwa hoja na kwa malumbano 
ambayo hayana maana bali yanaweza kuleta mitafaruku isiyokuwa ya lazima 
hasa kwa wale wanaoshindwa kwani wanapaswa kukubali matokeo. 
 Kwa
 upande wake Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa 
amesikitishwa na kifo cha marehemu ambaye alikuwa ni ndugu kwani 
wamekuwa wakiishi kama familia moja na walikuwa na ushirikiano mkubwa 
baina ya familia zao. 
 Ridhiwani
 alisema kuwa kifo hicho ni pigo kwa familia hiyo pia kwa Taifa kwani 
alikuwa ni mtumishi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na alikuwa 
mtaalamu wa rada hivyo pengo lake haliwezi kuzibika kikubwa ni kumwombea
 marehemu. 
Rais
 Dk Jakaya Kikwete alituma salamu za pole kwa familia hiyo kupitia kwa 
Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete na kusema kuwa anatoa pole
 na Mungu awape nguvu katika kipindi hichi kigumu cha maombolezo na yuko
 pamoja nao. 
 Alisema
 kuwa Rais alishindwa kuhudhuria msiba huo kwani kwa sasa yuko nje ya 
nchi lakini pindi atakaporudi ataitembelea familia hiyo kwa ajili ya 
kuifariji kufuatia kifo cha mtoto wa aliyekuwa kiongozi wa kabila 
wafugaji 
 Naye
 mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Demokrasia na 
Maendeleo (CHADEMA) Mathayo Torongei alisema ili amani iendelee kuwepo 
ni vema dola ikatenda haki badala ya kupendelea upande mmoja. 
 Marehemu
 alifariki kwa ajali baada ya gari alilokuwa akiendesha kupasuka tairi 
la mbele na kusababisha ajali iliyopelekea kifo chake siku ya Septemba 
16 mwaka huu  huko Mtwara. Ameacha mke na watoto watatu.
 Baadhi ya akinamama ambao ni ndugu wakaribu wakilia
Jeneza lenye mwili wa marehemu likiwa limebebwa na wanajeshi ukiwasili makaburini
 Baadhi ya Wazee wakiwa wamekaa kwenye msiba huo huko kijiji cha Maviyangombe Lugoba wilayani Bagamoyo.
 Kulia
 ni Ridhiwani Kikwete mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM 
akifuatiwa na mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga, mkuu wa wilaya ya
 Nachingwea Pololet Mgema na mgombea ubunge Jimbo hilo kupitia Chama Cha
 Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Matayo Torongei wakiwa kwenye msiba 
huo.
 Askofu Jacob Mameo Ole Paulo akizungumza wakati wa msiba huo.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni