SADIFA AWAPONGEZA VIJANA KWA MSHIKAMANO ARUISHA

Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa UVCCM taifa, Sadifa Juma Khamisi, amewapongeza vijana mkoani Arusha kwa mshikamano walionao katika kipindi hiki cha kampeni na mshikamano ambao unatoa imani kubwa kwa chama cha mapinduzi kupata ushindi kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Sadifa,ametoa pongezi hizo leo alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha shirikisho la vyuo vikuu mkoa wa Arusha kwa pamoja na baraza la UVCCM wilaya ya Arusha kilichofanyika ukumbi wa Chama cha Mapinduzi mkoa.

Sadifa,amewataka vijana wasilale bali waimarishe kampeni katik kipindi hiki ili chama cha mapinduzi kipate ushindi mkubwa kwenye uchaguzi mkuu ujao..

Amwataka makatibu wa UVCCM,mkoa na wilaya zote nchini kufanyia kazi kwa haraka pindi wanapopata taarifa za kuwepo matukio ya kuwakwamisha vijana kufanya kazi ikiwemo,kufanyiwa vurugu na  kushambuliwa na wanachama wa upinzani .

 Amewataka vijana kujipanga tayari kuwakabiri wanachama wa vyama vya upinzania ambao wanakusudia kuvuruga uchaguzi na kuwakumbusha kuwa vijana ndio walinzi wa chama cha mapinduzi.

Pia amewataka kufanya kampeni za kistaarabu ambazo zitawashawishi wapiga kura kukipigia chama cha mapinduzi kura na hivyo kuibuka na ushindi wa kishindo ila yeyote atakaye mchokoza mmoja wenu uvumilivu sio silaha ya vijana bali mjibu mapigo.

"Najua wamejipanga kuhakikisha kuwa wanaharibu uchaguzi nyie muwe wastaarabu katika kuhakikisha chama chetu kinapata ushindi kuanzia kwa dkta Magufuli hadi kwa madiwani wetu ifikapo oktoba 25"alisema Sadifa

Aidha mkutano huo wa ndani wa vijana jijini hapa uliofanyika katika ukumbi wa ccm mkoa uliibua hisia mbali mbali huku vijana wakitunishiana misuli hali iliyopelekea mwenyekiti huyo wa uvccm taifa kuweka sawa hali hiyo na mwisho kuondoka ukumbini hapa.

Sadifa alisema kuwa hali ya sasa ya kisiasa inavyoonekana wenzetu wamejipanga kuhakikisha uchaguzi unakuwa si wa amani lakini msiwafuate hadi pale watakapowachokoza ndiyo hapo vijana onyesheni kuwa nanyi ni vijana.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni