Katika
 hali isiyotarajiwa  na wengi katika Jimbo la Moshi Mjini, Mgombea 
Ubunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Davis Mosha ameanza utekelezaji
 wa ahadi zake katika Jimbo hilo,  wiki chache baada ya kuzungumza na 
wanamuziki na wasanii kuhusu kazi zao na wasanii hao kuomba kupata kituo
 cha Redio cha kisasa na Studio ya kisasa ambavyo vitaweza kufanya kazi 
zao kwa ubora zaidi na pia kufika mbali.
Katika
 kutekeleza hilo Mh. Davis Mosha amekwishaanza ujenzi wa Studio ya 
Kisasa ya Kituo cha Redio chini ya Kampuni yake ya Africa Swahili Media 
na ujenzi huo unatarajiwa kukamilika mapema na vifaa vya Studio huyo 
vinatarajiwa kuwasili muda wowote kutoka Dar es Salaam baada ya kuwasili
 Bandarini vikitokea Nchini Italy. Mh. Davis Mosha aliwaahidi wasanii 
hao kufungua kituo cha Redio kitakachoweza kusikika Tanzania Nzima na 
Duniani kote kwa njia ya Satelite. Pia aliwahakikishia kufungua na kituo
 cha televisheni. Kituo hicho cha Redio na Studio ya kisasa 
kianatarajiwa kufunguliwa katika jingo la Kilimanjaro Commercial Complex
 Maarufu kama jingo jipya la NSSF lililopo Moshi Mjini.
  | 
| Mh. Davis Elisa Mosha | 
  
  | 
| Hati ya Kontena la Vifaa vya Studio lililotoka Italy Baada ya kuingia Bandari ya jiji la Dar es Salaam. | 
Mbali 
na utekelezaji huo wa Kero ya Wasanii, Mh. Davis Elisa Mosha wiki 
iliyopita aliweza kufanya Ziara ya kimya kimya katika Soko la Mitumba la
 King George Memorial na kutazama Changamoto za Soko hilo lakini pia 
alipata fursa ya kuzungumza na uongozi wa Soko hilo na wafanyabiashara 
wa Soko hilo. Kwa pamoja walieleza MAzingira magumu wanayofanyia 
Biashara huku ikiwa Miundombinu mibovu ikiwemo vyoo na Soko halina Paa 
inapelelea iwapo mvua itanyesha basi kunakua hakuna biashara kabisa 
maana Bidhaa hunyeshwa na Mvua na mbali na Mvua pia jua ni lao. Katika 
kutatua changamoto hizo Davis Mosha aliwaahidi kulifanyia kazi mapema 
tatizo lao na hatosubiri mpaka muda wa uchaguzi ufike maana adha hiyo 
wanayoipata ni wananchi wa Moshi wakiwemo mama zake na baba zake waliopo
 hapo Sokoni. 
  | 
| Mh. Davis Mosha alipotembelea Soko la Mitumba la Memorial na kujionea changamoto mbalimbali. | 
  | 
| Mh. Davis Mosha akisalimiana na wafanyabiashara wa soko la Memoria alipotembelea soko hilo. | 
Kutokana
 na Ahadi hiyo Jana Mh. Mosha aliwasili Sokoni hapo na Mainjinia kutoka 
Kampuni ya Group Six ltd ambao ni Raia wa China   kwa lengo la kufanya 
kufanya vipimo na Michoro ya uboreahwaji wa Soko hilo ili kuweza kuondoa
 changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wa Soko hilo. Mainjinia hao 
walizunguka katika Soko hilo na kutazama eneo la Soko ili kuweka mipango
 ya kuanza ujenzi wa Soko hilo ambapo ujenzi huo hautoathiri 
wafanyabashara hao kuendelea kufanya biashara zao.
  | 
| Mainjinia
 Raia wa China kutoka Kampuni ya Group Six wakiwa soko la Mitumba la 
Memorial kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa Matengenezo ya soko hilo. | 
  | 
| Mh. Mwigulu Nchemba akimkaribisha Mh. Davis Mosha azungumze na Wafanyabiashara wa Soko la Memorial  | 
  | 
| Mh. Davis Mosha akizungumza na wafanyabiashara wa Soko la Mitumba la Memorial | 
Kutokana
 na utekelezaji huo wa ahadi wananchi mbalimbali wameonekana 
kufurahishwa na aina ya kiongozi waliompata ambaye anaomba Ridhaa ya 
kuchaguliwa kuongoza Jimbo la Moshi Mjini. Haata hivyo katika mkutano wa
 Hadhara uliofanyika jana katika Soko hili ulihudhuriwa na Viongozi 
mbalimbali wakiongozwa na Mh. Mwigulu Nchimbi ambaye alipata fursa ya 
kumzungumzia Davis Mosha. Mwigulu alisema kazi ngumu kuliko zote ni 
kutomchagua Davis Mosha kuwa Mbunge wa Moshi mjini na kazi Rais sana ni 
kumchagua Davis Mosha. Aliwaambia wakazi wa Moshi kuwa wana bahati ya 
kipekee kupata Mbunge ambaye ameanza utekelezaji wa ahadi zake kabla ya 
kusubiri bajeti ya serikali na viongozi kama hao ndi o Tanzania 
inawahitaji, Kwahiyo ikifika 25 mwezi wa Kumi wasifanye kosa wamchague 
Davis Elisa Mosha awe Mbunge wa Moshi Mjini pamoja na Madiwani wake wa 
ccm na bila kusahau kumpa kura za Kishindo Mgombea Urais wa ccm Ndugu 
John Pombe Magufuli.
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni