Mkuu 
wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akisalimiana na Maofisa wa 
Polisi katika Kanda Maalumu ya Tarime na Rorya jana wakati alipokuwa 
katika ziara ya kikazi katika mkoa huo wa Kipolisi.Kushoto ni Kamanda wa
 Polis Kanda Maalumu Tarime na Rorya, Lazaro Mambosasa.
 Mkuu 
wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akikata utepe kuashiria 
uzinduzi wa Hosteli ya Polisi Kanda Maalumu ya Tarime na Rorya jana 
wakati alipokuwa katika ziara ya kikazi katika mkoa huo wa Kipolisi.
 Mkuu 
wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akizindua Hosteli ya Polisi 
katika mkoa wa Kipolis Kanda Maalumu ya Tarime na Rorya jana wakati 
alipokuwa katika ziara ya kikazi katika mkoa huo wa Kipolisi
Mkuu 
wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akizungumza na wadau wa 
Polisi (hawapo pichani) wakati alipokuwa  katika ziara ya kikazi mkoa wa
 Kipolisi Tarime na Rorya ambapo alitumia kikao hicho kuwaasa kufanya 
uchaguzi kwa amani na utulivu.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi, Tarime.
Mkuu
 wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu amewataka Viongozi wa Vyama 
vya Siasa katika Wilaya za Tarime na Rorya kufanya Kampeni za Kistaarabu
 ili kufanikisha Uchaguzi Mkuu pamoja na kuimarisha Amani na Usalama 
Wilayani humo.
IGP
 Mangu aliyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na Wadau wa Polisi 
wakiwemo Viongozi mbalimbali, Vyama vya Siasa pamoja na Wagombea wa Viti
 vya Ubunge na Udiwani, wakati alipokuwa katika Ziara ya Kikazi katika 
Kanda Maaalum ya Polisi Tarime na Rorya.
Alisema
 ili uchaguzi wa mwaka huu uweze kufanyika kwa amani, Viongozi wa Vyama 
vya Siasa na Wagombea hawana budi kuwashawishi wafuasi wao kufuata 
Maadili ya Uchaguzi ikiwemo kutotoleana lugha za Matusi.
IGP
 Mangu alisema baada ya Uchaguzi maisha yataendelea kama kawaida hilo ni
 jukumu la Wananchi wote wa Tarime kuondoa Uhasama wao katika mambo ya 
Siasa kwa kuwa Siasa siyo Uhasama.
Aidha,
 aliwashauri Wagombea Ubunge na Udiwani katika Majimbo ya Tarime Mjini, 
Vijijini, na Rorya kukutana mara kwa mara ili kujenga kuaminiana na 
kutatua changamoto zinazojitokeza katika kipindi hiki cha kampeni na 
hatimaye siku ya uchaguzi Mkuu.
Kwa
 upande wake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Polisi Tarime na Rorya, 
kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Lazaro Mambosasa, aliwahakikishia Wadau
 wote kuwa Jeshi la Polisi limejipanga vyema kukabiliana na vitendo 
vyote vya vurugu vitakavyojitokeza, pamoja na kuhakikisha kila Mwananchi
 aliyejiandikisha anapata fursa ya kupiga kura bila vitisho vya aina 
yoyote.
Naye
 Mgombea Ubunge katika Jimbo la Rorya kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi,
 Lameck Airo alisema katika jimbo analogombea hakuna vurugu kwa kuwa 
wamekuwa wakiheshimiana katika Kampeni ili kuepusha vurugu kwa Wagombea 
na Wafuasi wao.
Kikao
 hicho kilihudhuriwa na Viongozi mbalimbali wakiwemo Viongozi wa 
Dini,Vyama vya Siasa, Wafanyabiashara, Asasi zisizo za Kiserikali, Wazee
 wa Kimila pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya
 Tarime.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni