Mratibu Mkazi wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez akizungumza wakati akizindua Malengo Endelevu 17 ya Maendeleo nchini
 (SDG’s) Tanzania katika  shule ya Uhuru mchanganyiko, katika hafla 
ambayo pia benki ya Standard Chartered Tanzania ilishiriki na  kugawa 
vitu mbalimbali kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo. (Picha na Zainul 
Mzige wa Modewjiblog)
Na Mwandishi wetu
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja 
wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro 
Rodriguez, amesema uondoaji umaskini nchini unawezekana kwa ushirikiano 
kati ya wadau mbalimbali wa maendeleo.
Kauli hiyo ameitoa mwishoni mwa wiki wakati akizindua Malengo Endelevu 17 ya Maendeleo nchini
 (SDG’s) Tanzania katika  shule ya Uhuru mchanganyiko, katika hafla 
ambayo pia benki ya Standard Chartered ilishiriki na  kugawa vitu 
mbalimbali kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo.
Katika hafla hiyo ambayo 
ilitengenezwa mahususi kuanzisha utekelezaji wa Malengo Endelevu (SDG’s)
 yakiwemo ya elimu, afya na mazingira Standard walipeleka miti 150 ya 
kupanda, kompyuta na pia kutumia muda kuangalia afya za wanafunzi.
Alisema katika kukabiliana na 
umaskini kwa kuangalia Maendeleo Endelevu hakuna kitu kigumu 
ukilinganisha na ugumu wa mwanafunzi asiyeona kujifunza kwa kupitia 
vitabu vya nukta nundu na asiyesikia kuwasiliana na mtu mwingine lakini 
pamoja na ugumu huo watoto hao wanaweza.
Alisema kwa ushirikiano wa wadau 
kama walivyofanya wao na benki ya Standard Chartered Tanzania anaamini 
kwamba maendeleo yatafikiwa na Tanzania itafanikiwa kuzika umaskini 
ifikapo mwaka 2030.
Alisema kutiwa saini kwa Malengo 
Endelevu na viongozi wa nchi 190 kumeonesha wazi nia ya seriakli 
mbalimbali duniani kushughulikia umaskini na kuuzika kwa kutekeleza 
malengo hayo endelevu.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole akitoa salamu za 
Mkurugenzi wake ambapo benki hiyo imeahidi kushiriki kikamilifu katika 
kuhakikisha utekelezaji wa malengo mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG's) 
yanafanikiwa nchini Tanzania. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez, Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa 
Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu (kulia) pamoja na Mkuu wa Mahusiano wa 
benki ya Standard Chartered Tanzania, Juanita Mramba (wa pili kulia).
Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi wa 
Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole, alisema kwamba 
ni lengo la benki hiyo ni kurejesha faida kwa jamii kupitia miradi yake 
mbalimbali na kwamba kusaidia shule hiyo ya Uhuru mchanganyiko 
iliyoanzishwa 01-01-1921 awali ikiitwa Government African secondary 
school kabla ya kuhamishiwa Mzumbe Morogoro 01-01-1953 na kubadilishwa 
jina kuwa Kichwele African boys middle school ikiwa na madarasa ya 
V-VII, ni sehemu ya kurejesha faida kwa jamii.
Alisema ni lengo la benki hiyo kwa 
mwaka huu kuwezesha kupatikana kwa dola za Marekani milioni 5 kusaidia 
mambo mbalimbali ya watoto kwa mwaka huu kwa nchi za Afrika mashariki 
huku Tanzania pekee watoto milioni 10 wakifikiwa.
Benki hiyo yenye matawi Dar es 
salaam, Mwanza na Arusha katika miradi yake ya afya, vijana na elimu 
wamekusudia kushirikiana na Umoja wa Mataifa kutekeleza malengo 
mbalimbali endelevu ikiamini kwamba jamii ikiboreshwa itakuwa katika 
mfumo mzuri wa maendeleo na kupiga vita umaskini.
Malengo ya SDG’s yamepangwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka 15.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi 
Uhuru mchangayiko, Anna Mshana akitoa risala fupi ya shule yake sambamba
 na changamoto zinazoikabili shule yake kwa ugeni huo kutoka Umoja wa 
Mataifa na Benki ya Standard Chartered Tanzania.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Anna 
Mshana alisema shule hiyo ambayo ilianzisha kitengo cha wanafunzi 
wasioona 1962 na kubadilishwa kuwa Shule ya msingi Uhuru mchanganyiko 
mwaka 1964, inakabiliwa na changamoto mbalimbali.
Miongoni mwa matatizo ni miundombinu
 ya shule hiyo isiyokidhi mahitaji halisi, ukosefu wa ukuta, mashine za 
kufundishia watoto wasioona, upungufu wa mabweni, magodoro, vitanda na 
gari la kuwakimbiza hospitalini inapotokea dharura.
Alisema ingawa kuna taasisi hutoa 
msaada wa gari na matibabu kwa watoto mchana, lakini nyakati za usiku 
kukitokea dhararu inabidi shule igharamie ingawaje wakati mwingine 
hatuna fedha inakuwa ni changamoto kwetu.
Alisema Shule ya msingi Uhuru 
mchanganyiko yenye kutoa elimu jumuishi  ina vitengo vya ufundi seremala
 (1975) wanafunzi wenye mahitaji maalumu ulemavu wa akili (1984) na 
viziwi na wasioona (Deafblidn) kilichoanzishwa mwaka 1994.
Wanafunzi ambao ni viziwi nao walipata fursa ya kuja kila kinachoendelea kutoka kwa mkalimani wao.
Mkuu wa Mahusiano wa benki ya 
Standard Chartered Tanzania, Juanita Mramba akitangaza wanafunzi 17  
ambao walishiriki shindano la kuhifadhi malengo mapya ya Maendeleo 
Endelevu (SDG's) wakati wa kukabidhi zawadi kwa wanafunzi hao wa shule 
ya Uhuru mchanganyiko.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez akikabidhi zawadi zilizotolewa na Benki ya Standard 
Chartered Tanzania kwa wanafunzi hao, sambamba na Mwakilishi wa 
Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole akimkabidhi Mwalimu 
Mkuu wa Shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko, Anna Mshana (wa pili 
kushoto) moja kati ya kompyuta tano zilizolotolewa na Benki hiyo ikiwa 
ni kama ishara ya utekelezaji wa lengo namba nne “Quality Education” 
wakati wa uzinduzi wa Malengo mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) 
uliofanywa na Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa kushirikiana na 
Umoja wa Mataifa katika shule ya msingi Uhuru mchanganyiko jijini Dar 
mwishoni mwa wiki. Kulia ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro 
Rodriguez na kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Shule ya msingi Uhuru 
Mchanganyiko, Bw. Abubakar Mwambungu wakishuhudia tukio hilo.
Kompyuta tano zilizotolewa na Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa shule ya Uhuru mchanganyiko.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole (wa tatu kushoto), 
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati), Mwalimu Mkuu wa
 Shule ya msingi Uhuru Mchangayiko, Anna Mshana (wa pili kushoto), 
Mjumbe wa bodi ya kamati ya Shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko, 
Abubakari Mwambungu (kushoto) pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Benki 
ya Standard Chartered Tanzania katika picha ya pamoja huku wakiwa 
wameshikilia  miche ya miti mbalimbali ikiwemo ya matunda ambapo zaidi 
ya miche 150 ya miti ilipandwa kuzunguka mazingira ya shule hiyo kulinda
 mazingira ikiwa ni ishara kwa vitendo ya  utekelezaji wa lengo namba 13
 "Climate Action" kati ya Malengo 17 mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG’s)
 nchini Tanzania.
Pichani juu na chini baadhi ya wanafunzi na walimu wa shule ya msingi Uhuru mchanganyiko waliohudhuria uzinduzi huo.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole sambamba na Mratibu 
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez wakishiriki zoezi la upandaji 
miti kuzunguka maeneo ya shule ya Uhuru mchanganyiko jijini Dar mwishoni
 mwa wiki.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez akishiriki zoezi la upandaji miti sambamba na baadhi ya
 wanafunzi wa shule Uhuru mchanganyiko.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi 
Uhuru Mchangayiko, Anna Mshana akitoa maelezo kwa Mratibu Mkazi wa 
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo 
(UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (aliyeinama) na Mkuu wa Mahusiano wa 
benki ya Standard Chartered Tanzania, Juanita Mramba (kulia) 
walipotembelea darasa la awali la watoto wenye ulemavu wa macho (upofu) 
katika shule hiyo. Nyuma ya Mwalimu Mkuu ni Mjumbe wa Kamati ya Shule ya
 Msingi Uhuru Mchangayiko, Abubakar Mwambungu.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez akicheza na mtoto Fatuma Haji wa darasa la awali katika
 shule hiyo ambaye ni mlemavu wa macho alipotembelea darasa hilo kabla 
ya kuzindua wa Malengo mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) hafla 
iliyoandaliwa na  Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa kushirikiana 
na Umoja wa Mataifa katika shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko jijini Dar
 mwishoni mwa wiki.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole, Mratibu Mkazi wa 
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo 
(UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, Mkuu wa Mahusiano wa benki ya Standard 
Chartered Tanzania, Juanita Mramba pamoja na ujumbe wao katika nyuso za 
masikitiko walipotembelea darasa la watoto wenye ulamavu wa macho 
(vipofu) na  matatizo ya kutosikia (viziwi) katika shule ya msingi Uhuru
 mchanganyiko.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole, Mratibu Mkazi wa 
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo 
(UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, Mkuu wa Mahusiano wa benki ya Standard 
Chartered Tanzania, Juanita Mramba na ujumbe wao katika picha ya pamoja 
na wanafunzi ambao ni walemavu wa macho ambao pia ni viziwi katika shule
 ya msingi Uhuru mchanganyiko.
Walimu wa darasa la watoto wenye ulemavu wa macho ambao ni viziwi wakicheza ngoma na wanafunzi wao.
Maana ya ulemavu wa macho na kuwa kiziwi.
Mkutubi wa maktaba ya shule ya 
Uhuru mchanganyiko, Masanja akitoa maelezo ya namna mashine za kukuzia 
maandishi kwa wale wanafunzi wenye uono hafifu katika shule hiyo kwa 
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, 
Charles Katongole (kushoto) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro 
Rodriguez walipotembelea maktaba hiyo.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez akipitia Katiba maalum kwa watu wenye ulemavu wa macho 
iliyopo kwenye maktaba ya shule hiyo. Kushoto kwake ni Mwakilishi wa 
Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez na Ujumbe wa Benki ya Standard Chartered Tanzania 
ulioongozwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered 
Tanzania, Charles Katongole wakitembelea mambweni ya wanafunzi katika 
shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole, Mratibu Mkazi wa 
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo 
(UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania katika picha ya pamoja na baadhi ya 
wanafunzi wa shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole (kulia) na Mratibu 
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na 
wanafunzi wa shule ya msingi Uhuru mchanganyiko Issa Abasi Wenge w 
darasa la pili (wa pili kushoto) mlemavu wa ngozi na Fatuma Haji  (wa 
pili kulia) wa shule ya awali mwenye ulemavu wa macho.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki
 ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole (kulia) na Mratibu 
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na Mwanafunzi Mariana Alex 
(Mariana the voice of the SDGs in TZ) wa darasa la tano katika shule ya 
msingi Uhuru mchanganyiko jijini Dar. #TELLEVERYONE about the #GlobalGoals 
Mtaalam wa Mahusiano na 
Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu akiserebuka na 
baadhi ya wanafunzi wa shule ya Uhuru mchangayiko.
Bango lililoorodhesha Malengo 17 mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG’s).
Siku ilimazika kwa mechi ya 
kirafiki baina ya Shule ya msingi Uhuru mchanganyiko na wafanyakazi wa 
Benki ya Standard Chartered Tanzania katika viwanja vya shule ya 
sekondari Benjamin Mkapa ambayo ilizinduliwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi
 wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole (kulia) na 
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni