BENKI YA CRDB YAZINDUA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA NA KUTOA VIFAA TIBA KWA MANISPAA YA KONONDONI

  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja uliofanyika jijini Dar es Salaam na kukabidhi vifaa tiba kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa kipindupindu katika Manispaa ya Kinondoni. (Picha na Francis Dande).
 Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja uliofanyika Dar es Salaam.
Baadhi ya Mameneja na Wakurugenzi wa Benki ya CRDB wakiwa katika hafla hiyo.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akikabidhi msaada wa vifaa tiba kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mhandisi Mussa Natty, kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa kipundupindu, ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Dk. Aziz Msuya na kulia ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB anayeshughulikia Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyopadhayay. (Picha na Francis Dande).
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akikabidhi msaada wa vifaa tiba kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mhandisi Mussa Natty, kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa kipundupindu, ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Dk. Aziz Msuya na wa pili kulia ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB anayeshughulikia Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyopadhayay. 
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akikabidhi msaada wa vifaa tiba kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mhandisi Mussa Natty, kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa kipundupindu, ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB anayeshughulikia Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyopadhayay na Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Dk. Aziz Msuya.
 Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika picha ya pamoja
 Baadhi ya maofisa wa Benki ya CRDB
 Vifaa tiba vilivyokabidhiwa leo.


  Na Mwandishi Wetu

BENKI ya CRDB imekabidhi dawa na vifaa tiba vyenye thamani ya sh. milioni 15 kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa kipindupindu katika Manispaa ya Kinondoni Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja.

Msaada huo ulitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk. Charles Kimei kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Injinia Mussa Natty aliyeishukuru benki hiyo na kukiri kwamba kipindupindu kipo katika manispaa yake.

Akizungumza baada ya kupokea dawa na vifaa tiba hivyo, injini Natty alisema mpaka sasa ugonjwa huo umepoteza maisha ya watu 17 katika manispaa hiyo huku wengine 1194 wameugua kipindupindu. 
“Kata zote 34 za manispaa ya Kinondoni zimeathirika na kipindupindu kilichoanzia Mwananyamala Agost 15 mwaka huu kata nyingine zenye ugonjwa huo ni Mburahati, Kigogo, Sinza, Mabibo, Magomeni, Kimara na Manzese.

"Mpaka sasa kambini kuna wagonjwa 25 nawashauri watanzania waache kusalimiana kwa kushikana mikono sababu ugonjwa huu unaendezwa kwa uchafu,” alisema injinia Natty.

Dk. Kimei alisema wiki ya huduma kwa wateja huadhimishwa kila mwaka na benki hiyo viongozi wa CRDB kutoa huduma kwenye matawi mbalimbali huku akieleza kwamba kaulimbiu ya mwaka huu ni Asanteni Sana.

“Wateja wetu ndio jambo la kila jema linalotokea kwetu… tunaitumia wiki hii kufungua milango na kusogea karibu zaidi na wateja ili kusikiliza maoni, mahitaji na ushauri wao, lengo ni kuwahudumia kwa ubora zaidi,” alisema Dk. Kimei.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni