TANZANIA YAHIMIZA USHIRIKIANO KATIKA KUWASAIDIA WAKIMBIZI

Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa Majadiliano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu dhana ya kuwalinda raia (R2P) majadiliano yaliyojielekeza katika kutathimini mafanikio na changamoto za utekelezi wa dhana hiyo ikiwa ni miaka kumi tangu kuasisiwa kwake.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, akizungumza wakati wa Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu dhana ya wajibu wa kuwalinda raia, ambapo alisema licha ya kuasisiwa kwa dhana hiyo dunia bado imeendelea kushuhudia maisha ya watu wasiokuwa na hatia yakiendelea kupotea kwa sababu tu Jumuiya ya Kimataifa inashindwa kutumiza wajibu wake kwa wakati.
Wakimbizi katika kambi moja nchini Tanzania, ambao jana jumanne akizungumza katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika UN Balozi Tuvako Manongi amesema kutoka na wimbi kubwa linaloendelea la wakimbizi kukimbilia mataifa mengine kutafuta usalama wao. Jumuiya ya kimataifa haina budi kushirikiana na bila kubagua katika kuwalinda na utoaji wa huduma na misaada ya kibinadamu kwa wakimbizi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni