HALMASHAURI YA WILAYA YA MERU YAPANDA MITI 7000,YAWEKA BIKONI YA MIKAPA VYANZO VYA MAJI

Mahmoud Ahmad, Arusha

HALMASHAURI ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha imepanda miti 7000 huku miti 500 ikipandwa katika kilele cha Siku ya Mazingira Duniani pamoja na kuweka bikoni katika mipaka inayozunguka vyanzo vya maji.

Juni tano ya kila mwaka huwa ni Siku ya Mazingira Duniani ambapo wadau mbalimbali huitumika kufanya kampeni na kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira.
Akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mazingira duniani Ofisa Mifugo Wilaya ya Meru Dk. Amani Sanga kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo amesema kuwa Tanzania kama ilivyo kwa nchi nyingi Barani Afrika na duniani imeendelea kuathirika kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa mazingira unaotokana na shughuli mbalimbali zikiwemo za kilimo, ufugaji na ujenzi.
Amesema kauli mbiu kwenye siku hiyo kwa mwaka huu inasema hivi "Mkaa ni gharama tumia nishati mbadala" ambapo ameifafanua inamaanisha jamii kuwa na urafiki endelevu na mazingira asilia.Kila mtu anapaswa kutambua, kufurahi, kujivunia na kulinda uzuri wa mazingira asilia na kuhamasishana ili kuyatunza na kuyahifadhi.
"Uharibifu huu wa misitu hutokana na shughuli za kilimo na ufugaji kwa njia zisizo endelevu. Uharibifu huu wa misitu unachangia pia kukosekana kwa mvua, kukauka kwa mito, mabwawa na uoto wa asili,"amesema .Amebainisha kazi ya kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira inahitaji ushirikiano wa wadau katika ngazi zote na si jukumu la Serikali peke yake.
Dk.Sanga ameongeza Halmashauri ya Wilaya ya Meru katika kuazimisha siku hiyo imepata ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo Bonde la pangani, mMali hai klabu,Kili flora, Mamlaka ya making mjimdogo wa uUsa River Pamoja na SUAMA. 
Hivyo amesema taasisi na asasi za kiraia zikishirikiana katika kutekeleza kikamilifu sheria na kanuni za uhifadhi wa mazingira nchini itasaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira.Kwa upande wa Ofisa Maendeleo ya Jamii wa Bonde la pangani Abraham Yesaya amesema kuwa jumla ya miti 7000 imepandwa katika kata 12 na kutoa elimu ya misitu katika shule zaidi ya 20.

Amesisitiza ni wajibu wa mamlaka katika ngazi mbalimbali ziwe na mipango bora ya ardhi, mikakati ya uhifadhi wa vyanzo vya maji, pamoja na udhibiti wa uvunaji holela wa misitu na ufugaji usio endelevu.Pia kutoa elimu juu umuhimu wa kutunza mazingira na faida zinazopatikana ili wananchi waunge mkono jitihada zinazofanywa katika kulinda na kuhifandhi mazingira kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Ngyani kilichopo katika kata ya Nkwaranga katika halmashauri hiyo Elishilia Mathayo amesema amefurahishwa na hatua ya kuwekwa bikoni katika mipaka ya vyanzo vya maji kwani hiyo itasaidia kuongeza ulinzi na watu kutoharibu vyanzo hivyo.
"Bikoni hizi zitasaidia kuonesha wananchi wanaofanya shughuli za kibinadamu kutambua mipaka yao ya kufanya shughuli bila kuingia kwenye vyanzo vya maji ambavyo vinastahili kulindwa na kila mmoja wetu,"amesema.
Afisa mifugo wa Meru Dkt. Amani Sanga akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani na wananchi wa kijiji cha Ngyani kilichopo katika kata ya Nkwaranga ndani ya halmashauri ya Meru .
Afisa Maendeleo ya Jamii wa bonde la pangani Abraham Yesaya akiwa anaelezea shughuli ambazo wanazifanya wao kama bonge la pangani
Mgeni rasmi akipanda moja ya miti 
Baadhi ya wadau wa SUAMA wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi mara baada ya kufanya shughuli ya upandaji miti
Mwenyekiti wa kijiji cha Ngyani kilichopo katika kata ya Nkwaranga katika halmashauri ya Meru, Elishilia Mathayo akizungumza katika maadhimisho hayo
mmoja wa wananchi ambaye jina lake halikufahamika akitoa dukuduku lake mbele ya mgeni rasmi ambapo aliomba zoezi hili la upandaji miti liwe endelevu 
mbali na upandaji miti pamoja na uelimishaji juu ya utunzaji wa mazingira pia halmashauri ya meru kwa kushirikiana na bonde la pangani waliandaa maonyesho ya majiko mbalimbali ambayo yanatunza mazingira kama kauli mbiu inavyosema mkaa ni gharama tumia nishati mbadala

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni