Mahmoud Ahmad, Arusha
HALMASHAURI
 ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha imepanda miti 7000 huku miti 500 
ikipandwa katika kilele cha Siku ya Mazingira Duniani pamoja na kuweka 
bikoni katika mipaka inayozunguka vyanzo vya maji.
Juni
 tano ya kila mwaka huwa ni Siku ya Mazingira Duniani ambapo wadau 
mbalimbali huitumika kufanya kampeni na kutoa elimu kuhusu umuhimu wa 
kutunza mazingira.
Akizungumza
 wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mazingira duniani Ofisa 
Mifugo Wilaya ya Meru Dk. Amani Sanga kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo 
amesema kuwa Tanzania kama ilivyo kwa nchi nyingi Barani Afrika na 
duniani imeendelea kuathirika kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa 
mazingira unaotokana na shughuli mbalimbali zikiwemo za kilimo, ufugaji 
na ujenzi.
Amesema
 kauli mbiu kwenye siku hiyo kwa mwaka huu inasema hivi "Mkaa ni gharama
 tumia nishati mbadala" ambapo ameifafanua inamaanisha jamii kuwa na 
urafiki endelevu na mazingira asilia.Kila mtu anapaswa kutambua, 
kufurahi, kujivunia na kulinda uzuri wa mazingira asilia na 
kuhamasishana ili kuyatunza na kuyahifadhi.
"Uharibifu
 huu wa misitu hutokana na shughuli za kilimo na ufugaji kwa njia zisizo
 endelevu. Uharibifu huu wa misitu unachangia pia kukosekana kwa mvua, 
kukauka kwa mito, mabwawa na uoto wa asili,"amesema .Amebainisha
 kazi ya kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuhifadhi 
mazingira inahitaji ushirikiano wa wadau katika ngazi zote na si jukumu 
la Serikali peke yake.
Dk.Sanga
 ameongeza Halmashauri ya Wilaya ya Meru katika kuazimisha siku hiyo 
imepata ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo Bonde la 
pangani, mMali hai klabu,Kili flora, Mamlaka ya making mjimdogo wa uUsa 
River Pamoja na SUAMA. 
Hivyo 
amesema taasisi na asasi za kiraia zikishirikiana katika kutekeleza 
kikamilifu sheria na kanuni za uhifadhi wa mazingira nchini itasaidia 
kupunguza kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira.Kwa
 upande wa Ofisa Maendeleo ya Jamii wa Bonde la pangani Abraham Yesaya 
amesema kuwa jumla ya miti 7000 imepandwa katika kata 12 na kutoa elimu 
ya misitu katika shule zaidi ya 20.
Amesisitiza
 ni wajibu wa mamlaka katika ngazi mbalimbali ziwe na mipango bora ya 
ardhi, mikakati ya uhifadhi wa vyanzo vya maji, pamoja na udhibiti wa 
uvunaji holela wa misitu na ufugaji usio endelevu.Pia
 kutoa elimu juu umuhimu wa kutunza mazingira na faida zinazopatikana 
ili wananchi waunge mkono jitihada zinazofanywa katika kulinda na 
kuhifandhi mazingira kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
Naye 
Mwenyekiti wa Kijiji cha Ngyani kilichopo katika kata ya Nkwaranga 
katika halmashauri hiyo Elishilia Mathayo amesema amefurahishwa na hatua
 ya kuwekwa bikoni katika mipaka ya vyanzo vya maji kwani hiyo itasaidia
 kuongeza ulinzi na watu kutoharibu vyanzo hivyo.
"Bikoni
 hizi zitasaidia kuonesha wananchi wanaofanya shughuli za kibinadamu 
kutambua mipaka yao ya kufanya shughuli bila kuingia kwenye vyanzo vya 
maji ambavyo vinastahili kulindwa na kila mmoja wetu,"amesema.
Afisa
 mifugo wa Meru Dkt. Amani Sanga akizungumza katika kilele cha 
maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani na wananchi wa kijiji cha 
Ngyani kilichopo katika kata ya Nkwaranga ndani ya halmashauri ya Meru .
Afisa
 Maendeleo ya Jamii wa bonde la pangani Abraham Yesaya akiwa anaelezea 
shughuli ambazo wanazifanya wao kama bonge la pangani
Mgeni rasmi akipanda moja ya miti 
Baadhi ya wadau wa SUAMA wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi mara baada ya kufanya shughuli ya upandaji miti
Mwenyekiti
 wa kijiji cha Ngyani kilichopo katika kata ya Nkwaranga katika 
halmashauri ya Meru, Elishilia Mathayo akizungumza katika maadhimisho 
hayo
mmoja
 wa wananchi ambaye jina lake halikufahamika akitoa dukuduku lake mbele 
ya mgeni rasmi ambapo aliomba zoezi hili la upandaji miti liwe endelevu 
mbali
 na upandaji miti pamoja na uelimishaji juu ya utunzaji wa mazingira pia
 halmashauri ya meru kwa kushirikiana na bonde la pangani waliandaa 
maonyesho ya majiko mbalimbali ambayo yanatunza mazingira kama kauli 
mbiu inavyosema mkaa ni gharama tumia nishati mbadala
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni