Na Mwamvua Mwinyi, Chalinze
JESHI la polisi 
mkoani Pwani, lina mshikilia Mariam Joakim mwenye miaka (52),kwa kosa la
 kudaiwa kusababisha kuteketeza kwa moto ofisi ya mbunge wa jimbo la 
Chalinze ,Bagamoyo Ridhiwani Kikwete .
Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Jonathan Shanna ,alithibitisha juu ya taarifa hiyo .
Alisema tukio hilo 
limetokea June 17 majira ya saa ya 18:00 ambapo jeshi hilo lilipokea 
taarifa kutoka kwa raia mwema kwa njia ya simu ,kuwa jengo la ofisi ya 
mbunge huyo inawaka moto.
“Katika tukio hilo ofisi yote imeteketea kwa moto na kuokolewa vitu vichache” alisema kamanda Shanna.
Kwa mujibu wa kamanda
 hiyo chanzo cha moto kimesababishwa na mtuhumiwa Mariam,ambae anaeleza 
aliwasha moto eneo la nyuma ya jengo hilo kwa lengo la kuchoma majani 
kisha moto ukamzidi na kushika majani na mabomba yaliyokuwa kando ya 
jengo hilo.
Anasema hatimaye moto uliunguza jengo lote.
Thamani ya uharibifu na vitu vilivyoungua haijajulikana na mtuhumiwa yupo mbaroni kwa mahojiano zaidi. 
Nae mbunge wa jimbo hilo ,Ridhiwani aliwashukuru wote walioguswa na mtihani alioupata.
“Mtihani unapita, 
asubuhi saa tano june 19 ,mungu akipenda nitakwenda angalia athari ya 
moto, na kueleza kwa ujumla tukio hili na hasara iliyotokea” alielezea 
Ridhiwani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni