ALIYESABABISHA OFISI YA RIDHIWANI KUTEKETEA KWA MOTO AKAMATWA


IMG-20180617-WA0062
Na Mwamvua Mwinyi, Chalinze
JESHI la polisi mkoani Pwani, lina mshikilia Mariam Joakim mwenye miaka (52),kwa kosa la kudaiwa kusababisha kuteketeza kwa moto ofisi ya mbunge wa jimbo la Chalinze ,Bagamoyo Ridhiwani Kikwete .
Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Jonathan Shanna ,alithibitisha juu ya taarifa hiyo .
Alisema tukio hilo limetokea June 17 majira ya saa ya 18:00 ambapo jeshi hilo lilipokea taarifa kutoka kwa raia mwema kwa njia ya simu ,kuwa jengo la ofisi ya mbunge huyo inawaka moto.
“Katika tukio hilo ofisi yote imeteketea kwa moto na kuokolewa vitu vichache” alisema kamanda Shanna.
Kwa mujibu wa kamanda hiyo chanzo cha moto kimesababishwa na mtuhumiwa Mariam,ambae anaeleza aliwasha moto eneo la nyuma ya jengo hilo kwa lengo la kuchoma majani kisha moto ukamzidi na kushika majani na mabomba yaliyokuwa kando ya jengo hilo.
Anasema hatimaye moto uliunguza jengo lote.
Thamani ya uharibifu na vitu vilivyoungua haijajulikana na mtuhumiwa yupo mbaroni kwa mahojiano zaidi. 
Nae mbunge wa jimbo hilo ,Ridhiwani aliwashukuru wote walioguswa na mtihani alioupata.
“Mtihani unapita, asubuhi saa tano june 19 ,mungu akipenda nitakwenda angalia athari ya moto, na kueleza kwa ujumla tukio hili na hasara iliyotokea” alielezea Ridhiwani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni