JUMUIA YA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI MUHIMBILI YAMUAGA MAREHEMU PROF. LEONARD LEMA


Wanataaluma wakiongozwa na Mkuu wa Idara ya Upasuaji wa MUHAS wakiandamana kusindikiza mwili wa marehemu Prof. Leonard Lema kuelekea graduation square, MUHAS kwa ajili ya tukio la kumuaga mwanataaluma mwenzao.
Viongozi mbalimbali wa MUHAS, MNH, MOI na JKCI wakisimama kwa heshima wakati mwili wa marehemu Prof. Leonard Lema ukiwekwa vizuri tayari kwa tukio la kumuaga
Mkuu wa Idara ya Upasuaji, MUHAS, Dkt. Larry Akoko akisoma wasifu wa marehemu maru tu baada ya mwili kuwasili kwenye graduation square MUHAS.
Viongozi mbalimbali taasisi na vyama vya kitaaluma wakitoa salamu za rambirambi wakati wa tukio la kuaga mwili wa Prof. Lema
Mke wa marehemu pamoja na watoto wake mara baada ya kupokea Tuzo ya Heshima iliyotolewa na Chama cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji Tanzania, kwa marehemu Prof. Leonard Lema kwa kutambua mchango wake katika kuendeleza Taaluma ya Upasuaji nchini. Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi, Muhimbili Prof. Appolinary Kamuahabwa akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Prof. Lawrence Museru wakipita kuaga mwili wa marehemu Prof. Leonard Lema.
Mke wa marehemu pamoja na watoto wake mara baada ya kupokea Tuzo ya Heshima iliyotolewa na Chama cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji Tanzania, kwa marehemu Prof. Leonard Lema kwa kutambua mchango wake katika kuendeleza Taaluma ya Upasuaji nchini.
Wanataaluma na wafanyakazi wengine wa sekta ya afya akiaga mwili wa marehemu Prof. Leonard Lema katika eneo la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi, MUHAS
Familia ya marehemu ikiaga mwili wa mpendwa wao Prof. Leonard Lema katika eneo la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi, MUHAS
Familia ya marehemu ikiaga mwili wa mpendwa wao Prof. Leonard Lema katika eneo la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi, MUHAS

Chuo Kikuu cha afya na Sayansi Shirikishi Muhmbili (MUHAS) pamoja na jumuia yote ya Hospitali ya taifa ya Muhimbi (MNH), Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo wameaga mwili wa marehemu Prof. Leonard Ellisa Lema, katika eneo la graduation square, MUHAS.

Tukio hili la kuaga mwili wa marehemu Prof. Lema lilitanguliwa na maandamano ya wanataaluma ili kumuenzi mwanataaluma mwenzao kwa mchango wake katika taaluma.

Pamoja na kutoa salamu za pole kwa familia ya marehemu kwa kuondokewa na mpendwa wao, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Appolinary Kamuhabwa alisema marehemu Prof. Leonard Lema atakumbukwa kwa moyo wake wa kujituma na kuchapa kazi kwa juhudi, maarifa na nidhamu. "Chuo na Taifa kwa ujumla limempoteza mtu ambaye alitoa mchango mkubwa katika sekta za Elimu ya Juu na Afya nchini hasa katika fani ya huduma za upasuaji" aliongeza Prof. Kamuabwa.

Pia katika tukio hili Chama cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji Tanzania, kimemtunukia marehemu Prof. Leonard Lema Tuzo ya Heshima kwa kutambua mchango wake katika kuendeleza Taaluma ya Upasuaji nchini. Tuzo hii ilikabidhiwa kwa Mke wa Marehemu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni