WATANZANIA ASILIMIA 90 WANATUMIA MKAA


mkaa matumizi
Na Mahmoud Ahmad,Dodoma.
ZAIDI  ya asilimia 90  ya watanzania  wanaokana kuishi kwa kutegemea nishati ya mkaa na kuni   kama chanzo kikuu cha kupikia .
Hata hivyo  nishati hiyo  inategemewa zaidi na wananchi  wenye kipato cha chini katika maeneo ya vijijini na mijini suala ambalo linapelekea ukataji wa miti kwa ajili ya mkaa kuwa mkubwa na  kusababisha umaskini.
Akizungumza jana na waandishi wa habari  ofisini kwake Afisa  misitu wa halmashauri ya  jiji la Dodoma Alexandra Kabado ametoa agizo kwa  wananchi mkoani hapa kutojihusisha na uchomaji misitu na kwamba  sheria itafuata mkondo wake kwa yeyote ambaye atabainika kujihusisha na uharibifu wa misitu.
,afisa misitu  huyo alisema kumekuwa na tabia sugu kwa baadhi ya watu kujihusisha na uchomaji  misitu kwa shughuli za kibinadamu  hali ambayo haikubaliki.
“Niwaambie wazi kuwa sheria itafuata mkondo wake kwa yeyote atakaye husika na uharibifu wa misitu kwa kuwa elimu imetolewa vya kutosha kama watu kusikia wamesikia kinachofanyika ni uzembe tu”alisisitiza.
Hata hivyo alisema,licha ya kuwepo faini ya shilingi elfu Hamsini kwa waharibifu wa misitu watu bado wanaendelea kujihusisha na uchomaji mkaa katika misitu na kukata miti kwa matumizi mengine.
Akieleza zaidi  Kabado aliongeza kuwa ukataji wa miti hovyo katika misitu  kunaweza kuleta majanga mbalimbali ikiwemo ukame na kusababisha uhaba wa mvua hali inayoleta uhaba wa chakula kwa baadhi ya maeneo. 
Aidha alisema  asilimia 75% mpaka 80% ya watanzania wanategemea kilimo na ufugaji na sehemu kubwa ya kilimo inategemea mvua hivyo kunapotokea  uhaba wa mvua shughuli za kilimo zinakuwa duni.
“ Uhaba wa mvua unasababisha mavuno kuwa haba na kusababisha njaa pamoja na umasikini hivyo kama maafisa misitu  tunasisitiza watu  kutumia nishati mbadala ili kuondokana na dhana ya ukataji misitu hovyo”alisema.
Hatahivyo, Afisa misitu huyo  amewataka wananchi hususani wakazi wa mkoa wa Dodoma  kutumia  nishati mbadala kama vile gesi na ikishindikana  kabisa  watumie majiko ambayo yanatumia mkaa kidogo pamoja na kuni ili kunusuru misitu  kwa maendeleo endelevu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni