Makamu wa
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan 
akimkabidhi Bw. Leonard Kushoka mfano wa hundi yenye thamani ya 
shiliningi za kitanzania milioni 300 mara baada ya kuibuka mshindi wa 
shindano la teknolojia ya nishati mbadala wa mkaa mwaka 2018, wengine 
pichani ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira 
Mhe. January Makamba na Mwenyekiti Mkazi wa Kampuni ya Shell Bw. Axel 
Knospe. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan 
akizindua ukuta uliojengwa kwenye kingo za Bahari ya Hindi pembezoni mwa
 barabara ya Barack Obama leo kuli ni  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
 Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba na Mwenyekiti Mkazi wa 
Kampuni ya Shell Bw. Axel Knospe. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia ukuta wa bahari
 wenye urefu wa mita 920 uliojengwa pembezomi mwa barabara ya Barack 
Obama mara baada ya kuizindua, mwingine pichani ni Waziri wa Nchi Ofisi 
ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba. (Picha na 
Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan 
akihutubia wakati wa uzinduzi wa ukuta uliojengwa  kwenye kingo za 
Bahari ya Hindi pembezoni mwa barabara ya Barack Obama leo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
 Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akihutubia uzinduzi wa 
ukuta uliojengwa kwenye kingo za Bahari ya Hindi pembezoni mwa barabara 
ya Barack Obama leo kulinda mazingira ya fukwe.
………………………………………………………………
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka Viongozi wa 
ngazi zote kuongeza nguvu katika utekelezaji wa Sera, Sheria, Mikakati 
na miongozo katika kukabiliana na uharibifu wa mazingira.
Makamu wa Rais wa ameyasema hayo 
wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo 
kitaifa yamefanyika jijini Dar es Salaam kwenye Viwanja vya Mnazi mmoja.
“ Ni muhimu, mipango ya maendeleo
 katika kukabiliana na uharibifu wa mazingira ili nchi yetu iwe na 
maendeleo endelevu” alisema  Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais amesema kazi ya 
kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa hifadhi ya mazingira unahitaji 
ushirikiano wa wadau wote kwa ngazi zote.
Maadhimisho ya Kimataifa 
yanafanyika India katika mji wa New Delhi yakibeba ujumbe wa kuhimiza 
kupunguza uchafuzi wa mazingira kutokana na matumizi ya bidhaa za 
plastiki (Beat Plastic Pollution) lakini hapa nchini Kitaifa ujumbe wa 
maadhimisho ni  “Mkaa Gharama: Tumia Nishati Mbadala”
Mapema leo, Makamu wa Rais 
alizindua ukuta wa bahari uliopo kwenye barabara ya Barack Obama wenye 
urefu wa mita 920, ukuta huo ambao umejengwa kuzuia bahari kuingia nchi 
kavu unakadiriwa kuwa na maisha kati ya miaka 70 mpaka 100 kutoka sasa.
Makamu wa Rais amesema kuwa 
Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kujenga uchumi wa Viwanda  na zipo
 faida nyingi za hifadhi na usimamizi zitakazotokana na Tanzania kuwa na
 Viwanda.
Mwisho, Makamu wa Rais amesema 
katika kufanikisha suala zima la uhifadhi wa Utunzaji wa mazingira mi 
lazima tuifanye kila siku iwe siku ya Mazingira.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni