*Ataka apewe majina ya watakaokiuka agizo hilo
*Akataza magari ya Serikali kulala nyumbani kwa mtu
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa 
amewaagiza watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Bahi mkoani Dodoma 
wanaoishi nje ya eneo lao la kazi wawe wamehamia ifikapo Julai 30, mwaka
 huu.
“Tunataka watumishi wa umma 
wawajibike na waishi katika vituo vyao vya kazi. Nawataka watumishi wote
 wa wilaya hii wanaoishi Dodoma wawe wamehamia hapa ifikapo Julai 30 
mwaka huu na wasiohamia nipewe majina yao,” amesisitiza.
Pia ameagiza magari yote ya 
Serikali baada ya kuisha muda ya kazi yawe yameegeshwa kwenye ofisi za 
halmashauri na ni marufuku kwa magari hayo kulala nyumbani kwa mtu.
Ametoa maagizo hayo leo 
(Jumatano, Juni 27, 2018) wakati akizinduavituo 51 vya kufuatilia 
taarifa za hali ya hewa, vituo 15 vya haidrolojia, kanzidata ya taarifa 
za hali ya hewa na kituo cha operesheni na mawasiliano ya 
dharura wilayani Bahi, Dodoma.
Waziri Mkuu amesema Serikali 
inataka watumishi wote wa umma nchini waishi kwenye vituo vyao vya kazi 
ili waweze kuwahudumia wananchi kwa ukaribu katika maeneo husika.
Katika hatua nyingine, Waziri 
Mkuu amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bahi, Bibi. Rachel
 Chuwa aanzishe mradi wa upimaji wa viwanja na viuzwe kwa watumishi na 
wananchi kwa gharama nafuu.
Waziri Mkuu amesema ni vema 
wilaya hiyo ikachangamkia fursa ya Serikali kuhamia Dodoma kwa kuboresha
 miundombinu mbalimbali ikiwemo nyumba za kuishi, hoteli na sehemu za 
burudani ili watumishi waliohamia Dodoma wapate sehemu za kujipumzisha 
pindi wamalizapo majukumu yao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni