Na Ahmed Mahmoud
Sheria mbali mbali zimekuwa 
zikitungwa kuhusiana na utunzaji wa mazingira lakini bado kumekuwa na 
ombwe la uharibifu na ukataji mkubwa wa misitu hapa nchini na kupelekea 
mabadiliko ya tabianchi je tatizo lipo wapi ni kwenye ufutaliaji wa 
sheria au elimu kwa wanchi haijawafikia.
Utaona pindi yanapotokea majanga 
mbali mbali hapa nchini ndipo kauli mbali mbali zinatoka mifano ipo 
mingi yakiwemo magonjwa ya milipuko mafuriko bila kuandaa mazingira yetu
 kabla ya kuharibika suala hili ndio chanzo kikubwa cha uharibifu wa 
mazingira hapa nchini.
Tarehe 5 ya mwezi wa sita  kila 
mwaka duniani kote husherehekea siku ya mazingira Duniani na nchini siku
 hiyo husherehekewa kwa upandaji wa miti na utoaji wa elimu ya utunzaji 
wa mazingira sanjari na matamasha,maonyesho na mikutano ya hadhara lengo
 kuu ni kufikisha ujumbe wa siku hiyo.
Sote ni muhimu kutambua 
kuadhimishwa kwa siku hii ya mazingira duniani kwani siku ya mazingira 
duniani ni siku iliyopangwa kimataifa ili kutoa fursa ya kukuza uelewa 
wa jamii na kuchukuwa hatua za maksudi za kuhifadhi na kutunza mazingira
 kwa ustawi wa maisha ya kizazi cha sasa na vijavyo.
Tatizo la uharibifu wa mazingira 
ni la ulimwengu wote ambalo linatokana na kuongezeka kwa shughuli mbali 
mbali za kimaendeleo katika Nyanja za kiuchumi na kijamii ambazo 
zimesababisha uchafuzi wa mazingira na kuathiri maisha ya mwanadamu na 
viumbe vingine.
Hali hii ya uchafuzi wa mazingira 
imesababisha majanga mbali mbali ya kimazingira na kijamii kama mafuriko
 na kuenea kwa hali ya jangwa ambayo ni matokeo ya mabadiliko ya 
tabianchi.
Matokeo haya yanasababishwa na 
binadamu hasa mataifa yalioendelea kiuchumi yanapofanya shughuli za 
kiuchumi na maendeleo bila kuwaza matokeo ya shughuli hizo kwenye 
mazingira na uharibifu wake.
Aidha  Afisa mazingira jiji la 
Dodoma Ally Mfinanga Kujisahau kwetu ndio kumetufanya binadamu kuwa 
waathirika wa mafanikio yetu mwenyewe(the victim of his own succer’) na 
dunia inalia kwa sababu ya madhara yaliojitokeza baada ya mwanadamu 
kujitenga na mazingira.
Amesema kuwa Uchafuzi huu 
unatokana na mambo makuu mawili,uzalishaji wa taka unaozidi uwezo wa 
mazingira kuhimili taka hizo hasa taka za plastiki jambo hili 
linahusisha kauli mbiu ya kimataifa ya mwaka huu inayosema kuwa
“ pambana na uchafuzi wa mazingira
 unaotokana na taka hasa za plastic’’ hii itaondoa tatizo lilopo la 
kuteketeza taka ngumu zilizoenea katika makazi yetu” alisema Mfinanga
Taka hizi za Plastiki zimekuwa ni 
kero kubwa ya uharibifu wa mazingira katika jamii nyingi  zinazozalisha 
taka hizi zina madhara mbali mbali ya kijamii na kimazingira kama 
ifuatavyo “uharibifu wa hewa(dioxine anda furans)unatokakana na 
kuunguzwa kwa plastik’
Uchafuzi wa vyanzo vya maji kama 
vile mito maziwa na bahari ambapo taka hizi huathiri mazalia ya viumbe 
wa majini hususani samaki na kuhatarisha maisha ya wanyama wanapokula 
plastiki hufa.
Taka hizi pia huharibu miundo 
mbinu ya maji mfano  mabomba na mifereji ya kupitishi maji kwa 
kusababisha kuziba hali hii ni moja ya uharibufu wa mazingira,kuharibu 
muonekano wa mazingira hasa maeneo ya wazi na kando kando ya barabara.
Narudia Kauli mbiu ya kitaifa 
 mwaka huu “mkaa ni gharama tumia nishati mbadala” utaona matumizi ya 
mkaa ndio imekuwa nishati mbadala hapa nchini huku wataalamu wakitoa 
nasaha mbali mbali yakupunguza matumizi ya nishati hiyo.
Kama tutachukuwa hatua za maksudi 
kuhakikisha tunabadili mwelekeo wa matumizi ya mkaa na kuangalia nishati
 mbadala tutaepuka na kuiepusha nchi kuingia katika mabadiliko ya 
tabianchi yanayotokana na shughuli zetu za kiuchumi.
Siku hii hapa nchini kitaifa 
ilifanyika jijini Dar es salaam na mkoani Dodoma yalipo makao makuu ya 
nchi yalifanyika kwenye viwanja vya Nyerere ambapo mgeni Rasmi alikuwa 
Naibu Meya wa Jiji Hilo Jumanne Ngede ambaye aliwataka watumishi wa 
halmashauri hapa nchini kuanza kujitathimini kama wamefikia malengo ya 
serikali katika suala zima la utunzaji wa mazingira katika halmashauri 
zao.
Kwa upande wake kaimu mkurugenzi 
 wa jiji la Dodoma Dickson Kimaro ambaye ni Afisa mazingira wa jiji hilo
 anasema kuwa wamejipanga kuhakikisha Sheria zinafuatwa na 
watakaobainika wanavunja sheria hatua kali zitachukuliwa iliwamo faini 
ya 50,000 au kupandishwa mahakamani au vyote kwa pamoja.
Amesema kuwa matumizi ya 
rasilimali za kimazingira kupita uwezo wake kujirejeza jambo 
hilolinahusisha kauli mbiu ya kitafa inayotanabaisha kuwa mkaa gharama 
tumia nishati mbadala ambayo itaokoa uharibifu wa misitu yetu.
Amesema kuwa ilimu wataendeleo 
kuitoa na kuwa atakaye mpeleka mtuhumiwa wa uchafuzi na uharibifu wa 
mazingira tapewa asilimia 50% ya fedha ya faini na kuwataka wananchi 
pamoja na askari jamii kuhakikisha watandea kazi hiyo kwa uweledi.
Kutokana na kauli hiyo ya Mh.Ngede
 inatukumbusha kwamba mahitaji yetu ya msingi yanatokana na rasilimali 
zilizoko kwenye mazingira ikihusisha hitaji muhimu la nishati ya 
kuni\mkaa ambazo zinatumiwa na wananchi wengi katika maeneo ya mjini na 
vijijini.
Hapa tunaona miti ni rasilimali 
muhimu sana kwa uhai na ustawi wa mwanadamu maana inahifadhi vyanzo vya 
maji na kusafisha hewa tunayovuta ili tuendelee kupata maji na kuvta 
hewa safi tunahitaji utunzaji wa misitu.
Hapa nchini kumekuwepo na ufyekaji
 wa uoto hasa misitu uliopitiliza uwezo wake wa kujirejeleza na matokeo 
tunetengeneza mazingira ya kuenea kwa hali ya jangwa hasa maeneo mbali 
mbali ambayo hapo awali yalikuwa ni vyanzo vikubwa vya maji.
 Muhimu elimu ikatolewa kwa jamii 
juu ua umuhimu wa hifadhi ya isitu ambao kazi yake kubwa ni kufyonza 
hewa ya ukaa(green house gas) ambayo ni chanzo kikuu cha mabadiliko ya 
tabianchi na uharibifu wa mazingira.
Rai yangu kwamba sote kwa pamoja 
tuwajibike kupanda na kutunza miti tutumie nishati mbadala na 
kuhakikisha taka zinatupwa katika hali iliyo salama kiafya na 
kimazingira ili vizazi vijavyo virithi hali tuliyoikuta sisi
Kama taifa sheria ziwekewe mkazo 
kama kwenye Halmashauri ya manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro 
walivyofanikiwa kuweka mji wao katika hali ya usafi na iwe tabia yetu 
isiwe nguvu ya soda mpaka kila jumamosi ya mwisho wa mwezi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni