Mkurugenzi wa Idara ya Jinsia, 
Wazee na Watoto wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA), 
Mohamed Shabani (wapili kulia) akimkabidhi Kamishna Jenerali wa Jeshi la
 Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye tuzo ya cheti cha heshima, kwa 
mchango wao katika kupambana na majanga ya moto na uokoaji. Hafla hiyo 
imefanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam. 
Kamishna Jenerali wa Jeshi la 
Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye, akionesha zawadi ya fulana ya 
mabalozi wa Taasisi ya Salama Salimini aliyokabidhiwa na Mkurugenzi wa 
Idara ya Jinsia, Wazee na Watoto wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo 
Tanzania (AWAMATA), Mohamed Shabani (kushoto), kama alama ya kutambua 
mchango wao katika kupambana na majanga ya moto na uokoaji, (kulia) ni 
balozi wa Salama Salimini Mwinyi Mangara. Hafla hiyo imefanyika Makao 
Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la 
Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye, akifafanua jambo kwa Waandishi 
wa habari (hawapo pichani) baada ya kukabidhiwa tuzo ya cheti cha 
heshima kutoka kwa Idara ya Jinsia, Wazee na Watoto wa Asasi ya 
Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA), kwa mchango wao katika 
kupambana na majanga ya moto na uokoaji. Hafla hiyo imefanyika Makao 
Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la 
Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (wa tatu kulia) akiwa na Viongozi
 Waandamizi wa Jeshi pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Jinsia, Wazee na 
Watoto wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA), Mohamed 
Shabani (wapili kushoto), (kulia) Kamishna wa Operesheni wa Jeshi hilo 
Billy Mwakatage, (kushoto) Kamishna wa Usalama Dhidi ya moto Jesuald 
Ikonko na (wapili kulia) ni balozi wa Salama Salimini Mwinyi Mangara. 
Hafla hiyo imefanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam. 
Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji
…………….
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji 
limepokea tuzo ya cheti cha heshima kwa kutambua mchango wao katika 
kupambana na majanga ya moto na uokoaji hapa nchini kutoka katika 
Taasisi ya Wazalendo na Maendeleo. Tuzo hiyo imepokelewa na Kamishna 
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye Makao Makuu 
ya Jeshi hilo yaliyopo Dar es salaam
Akizungumza Kamishna Jenerali 
baada ya kupokea tuzo ya cheti hicho. Alisema, anawashukuru Taasisi hiyo
 kwa kulipa Jeshi hilo tuzo hiyo kwa kazi nyingi ambazo taasisi hiyo 
imezifanya kwa kushirikia na Jeshi hilo ikiwepo kampeni ya kuitangaza 
namba ya simu ya dharura 114.
Kamishna Jenerali Andengenye, 
amezitaka Taasisi nyingine kushirikiana na Jeshi hilo katika kuzifufua 
Fire Hydrant zilizo haribika na zilizofukiwa ili kuongeza idadi ya vifaa
 hivyo ambayo ni msaada mkubwa wakati wa majanga ya moto. ‘‘Jamii 
ishirikiane na Jeshi letu katika kuvilinda visima hivyo (Fire Hydrant) vilivyopo mitaani kwani ni msaada mkubwa pale majanga ya moto yanapotokea’’.
Ni vema sasa mamlaka 
zinazoshughulikia miundombinu ya maji safi kwenye miji na majiji 
ikazingatia wanapotengeneza miundo mbinu hiyo, wakumbuke kuweka na 
mifumo ya maji ya zimamoto Fire Hydrant, pamoja na kuhakikisha wamiliki 
wanaojenga majengo makubwa na madogo wanaweka mifumo hiyo ya maji.
Tuna changamoto kubwa kwa upande 
wa visima hivyo, kwa hiyo kamapeni yetu ya kufufua na kuongeza visima 
hivyo vitasaidia kuleta tija katika utendaji kazi katika fani yetu. 
Tunashirikiana na Mamlaka za Maji kuhakikisha miundo mbinu hiyo inarudi 
na kutoa ushauri pale miradi mipya ya maji inapo jengwa.
Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya 
Wazalendo na Maendeleo Tanzania Bw. Muhammad Shaban alisema wamechukua 
uamuzi huo wa kutoa Tuzo hiyo kutokana na kuona mchango mkubwa wa Jeshi 
hilo walioutoa katika jamii. Pia amesema wataendea kutoa ushirikiano na 
Jeshi hilo katika utoaji elimu kwa umma. “Tupo tayari kushirikiana na 
Jeshi hili kuwaonesha sehemu zote ambazo fire hydrant zilizopo Mkoa wa 
Dar es salaam.”
“Kampeni ya kufufua fire hydrant 
imetugusa sana na kuona hatua hiyo ni msaada mkubwa kwa jamii kwani 
zitasaidia magari ya zimamoto na uokoaji kupata maji eneo la karibu 
majanga ya moto yanapotokea.”
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni