Spika wa Bunge la Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai (Mb), akizungumza wakati wa kikao 
cha 52 cha Bunge la 1 leo tarehe 18 Juni, 2018 Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
 Bajeti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Hawa Ghasia 
akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo kuhusu Bajeti ya mwaka wa fedha 
2018/19 wakati wa kikao cha 52 cha Bunge la 11 leo tarehe 18 Juni, 2018 
Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza akijibu swali wakati wa
 kikao cha 52 cha Bunge la 11 leo tarehe 18 Juni, 2018 Jijini Dodoma.
Mbunge wa Jimbo la Missungwi 
mkoani Mwanza, Mhe. Charles Kitwanga akichangia hoja kuhusu taarifa ya 
hali ya uchumi na mapendekezo ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 
2018/19 wakati wa kikao cha 52 cha Bunge la 11 leo tarehe 18 Juni, 2018 
Jijini Dodoma
Naibu Waziri wa Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza akiteta jambo na Mbunge
 wa Viti Maalum mkoa wa Singida, Martha Mlacha wakati wa kikao cha 52 
cha Bunge la 11 leo tarehe 18 Juni, 2018 Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya 
Rais Tawala za Mikoa na Seriikali za Mitaa (OR -TAMISEMI), Mhe. Joseph 
Kakunda akijibu swali wakati wa kikao cha 52 cha Bunge la 11 leo tarehe 
18 Juni, 2018 Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. 
Phillip Mpango(kulia)na Naibu wake Dkt. Ashatu Kijaji wakifuatilia hoja 
za wabunge kuhusu taarifa ya hali ya uchumi na mapendekezo ya Bajeti Kuu
 ya Serikali kwa mwaka 2018/19 wakati wa kikao cha 52 cha Bunge la 11 
leo tarehe 18 Juni, 2018 Jijini Dodoma. (Picha zote na: Frank Shija – 
MAELEZO, Dodoma)
 ………………………………………………………………………..
Na: Jonas Kamaleki-MAELEZO, Dodoma
Mbunge wa Viti Maalum, Chama cha 
Wananchi (CUF), Mhe.Rukia Kassim amepongeza juhudi za Serikali katika 
kukuza uchumi ikiwemo kuongezeka kwa pato la Taifa.
Mhe. Rukia ameyasema hayo leo 
Bungeni, Jijini Dodoma wakati akichangia mapendekezo ya Serikali kuhusu 
makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2018/19.
“Naipongeza Serikali kwa hatua za kukuza uchumi  hasa ukuaji wa Pato la Taifa unaotarajiwa kuwa asilimia 7.2”, alisema Rukia.
Naye Mbunge wa Urambo, Mhe. 
Margreth Sitta ameipongeza Serikali kwa kupendekeza kusamehe Kodi ya 
Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye taulo za kike.
“Mheshimiwa Spika hatua hii ya 
kusamehe kodi hiyo itapunguza bei ya taulo hizo ambayo itawafanya 
wanafunzi wa kike kuzipata kwa bei nafuu na kuwawezesha kuhudhuria 
masomo kwa muda wote wa masomo ikilinganishwa walivyokuwa wakishindwa 
kufanya hivyo wakiwa katika siku zao kwa kukosa taulo”,alisema Mama 
Sitta.
Akichangia kwenye bajeti kuu ya 
Serikali, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Mhe. Peter Serukamba amesema kuwa 
anampongeza saa Rais John Pombe Magufuli kwa kujenga miradi mikubwa 
miwili ya Standard Gauge naye Umeme wa Stiegler’s Gorge.
“Historia itamwandika Rais 
Magufuli kwa kazi kubwa anazofanya hasa kwa ujenzi wa miradi mikubwa 
nchini, ule wa reli ya Kisasa (Standard Gauge) na ule umeme wa 
Stiegler’s Gorge”, alisema Serukamba.
Aliongezea kuwa bajeti hiyo ni nzuri sana na inapaswa kuungwa mkono kwani inawajali wananchi.
Wabunge wanaendelea kuchangia 
bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/19 ambayo iliwasilishwa wiki 
iliyopita na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango.
Mwisho
Upinzani Wapongeza Juhudi za Serikali Kukuza Uchumi
Na: Jonas Kamaleki-MAELEZO, Dodoma
Mbunge wa Viti Maalum, Chama cha 
Wananchi (CUF), Mhe.Rukia Kassim amepongeza juhudi za Serikali katika 
kukuza uchumi ikiwemo kuongezeka kwa pato la Taifa.
Mhe. Rukia ameyasema hayo leo 
Bungeni, Jijini Dodoma wakati akichangia mapendekezo ya Serikali kuhusu 
makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2018/19.
“Naipongeza Serikali kwa hatua za kukuza uchumi  hasa ukuaji wa Pato la Taifa unaotarajiwa kuwa asilimia 7.2”, alisema Rukia.
Naye Mbunge wa Urambo, Mhe. 
Margreth Sitta ameipongeza Serikali kwa kupendekeza kusamehe Kodi ya 
Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye taulo za kike.
“Mheshimiwa Spika hatua hii ya 
kusamehe kodi hiyo itapunguza bei ya taulo hizo ambayo itawafanya 
wanafunzi wa kike kuzipata kwa bei nafuu na kuwawezesha kuhudhuria 
masomo kwa muda wote wa masomo ikilinganishwa walivyokuwa wakishindwa 
kufanya hivyo wakiwa katika siku zao kwa kukosa taulo”,alisema Mama 
Sitta.
Akichangia kwenye bajeti kuu ya 
Serikali, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Mhe. Peter Serukamba amesema kuwa 
anampongeza saa Rais John Pombe Magufuli kwa kujenga miradi mikubwa 
miwili ya Standard Gauge naye Umeme wa Stiegler’s Gorge.
“Historia itamwandika Rais 
Magufuli kwa kazi kubwa anazofanya hasa kwa ujenzi wa miradi mikubwa 
nchini, ule wa reli ya Kisasa (Standard Gauge) na ule umeme wa 
Stiegler’s Gorge”, alisema Serukamba.
Aliongezea kuwa bajeti hiyo ni nzuri sana na inapaswa kuungwa mkono kwani inawajali wananchi.
Wabunge wanaendelea kuchangia 
bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/19 ambayo iliwasilishwa wiki 
iliyopita na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango.
Mwisho
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni