JAFO ATOA WIKI MBILI KWA WAKURUGENZI KUBAINISHA MAENEO YA UJENZI WA MADARASA




 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akitoa maagizo kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa  wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa leo yaliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Jijini Dodoma.
 Mkurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Dkt. Charles Mhina akiongea na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kwenye mafunzo ya siku mbili kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa leo yaliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Jijini Dodoma.
 Baadhi ya Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo (hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa leo yaliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo (hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa leo yaliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Jijini Dodoma
 
………………………………………..
Na. Angela Msimbira  OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo ametoa wiki mbili kuanzia leo  kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa  nchini kuhakikisha wanabainisha  maeneo ya ujenzi  na  mafundi watakaojenga  madarasa 478 na mabweni 269.
Ameayasema hayo alipokuwa akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa leo yanayofanyika katika ukumbi wa chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Jijini Dodoma.
 Mhe. Jafo alisema kuwa tayari Serikali  imetenga shilingi bilioni 29 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 478 mapya na Mabweni 269 ili  kuhakikisha wananfunzi wote waliokosa  nafasi ya kupangiwa kujiunga na kidato cha tano awamu ya kwanza wanapata katika uchaguzi wa awamu ya pili.
Mhe. Jafo amewataka Wakurugenzi hao kuhakikisha wanatumia muda mdogo   kubainisha maeneo yatakayojengwa madarasa na mabweni kwa kutumia njia ya “Force Account” ili uchaguzi wa wanafunzi awamu ya pili uatakapofanyika na ujenzi huo uwe umekamilika. 
Mhe. Jafo aliwaagiza Wakurugenzi hao kusimamia ujenzi huo  na kuhakikisha unakamilika  tarehe 30/08/2018 ili  wanafunzi waliokosa nafasi ya kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya kwanza  wanachaguliwa katika awamu ya pili na kutimiza ndoto za wanafunzi hao .
Mhe Jafo aliwaagiza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini kuhakikisha wanasimamia kwa weledi ujenzi wa miradi mbalimbali katika Halmashauri zao ikiwemo ya ujenzi wa madarasa na Mabweni ili kupunguza changamoto ya ukosefu wa madarasa nchini.
“Ninawaagiza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Nchini  kuhakikisha wanasimamia ipasavyo ujenzi wa madarasa na mabweni kwa umakini wa hali ya juu ili dhamani ya fedha inayotolewa na Serikali iendane na  majengo yatakayojengwa. Alisema Jafo
Aidha Mhe. Jafo alisema sambamba na ujenzi huo Serikali imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya  vingine 98 na kuwataka kuhakikisha wanafanyakazi kwa weledi na umakini wa hali ya juu hasa katika suala zima la usimamizi wa miradi mbalimbali  ili dhamani ya fedha zinazotolewa iendane  na majengo yatakayojengwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni