Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akizungumza na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge Bungeni jijini
 Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akizungumza na Mbunge wa Kijitoupele Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha 
Bungeni jijini Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri 
Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenyeulemavu 
Jenista Mhagama, akijadili jambo na Waziri wa Elimu Profesa Joice 
Ndalichako, Bungeni jijini Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya 
Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu Kassim 
Majaliwa, akizungumza na Waziri wa Elimu Profesa Joice Ndalichako, 
Bungeni jijini Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim 
Majaliwa, akisalimiana na Makamu wa Rais wa Bunge la 
Afrika, Stephen Masele ambaye ni Mbunge wa Shinyanga Mjini, ofisini 
kwake Bungeni mjini Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri 
Mkuu) 
Waziri Mkuu Kassim 
Majaliwa, akizungumza na Makamu wa Rais wa Bunge la 
Afrika, Stephen Masele ambaye ni Mbunge wa Shinyanga Mjini, ofisini 
kwake Bungeni mjini Dodoma, kutoka kushoto ni Mbunge wa Mbozi 
Magharibi Mheshimiwa David Silinde na Mbunge wa Viti Maalum Zanzibar 
Asha Abdullah Juma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa 
amefanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa 
Stephen Masele na kumuahidi kwamba Serikali itampa ushirikiano ili aweze
 kutimiza majukumu yake.
Ametoa ahadi hiyo leo (Jumanne, 
Juni 5, 2018) wakati akizungumza na Mheshimiwa Masele ofisini kwake 
Bungeni, Dodoma. Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kumpongeza kwa 
kuchaguliwa kushika wadhifa huo.
Amesema ushindi wake katika 
nafasi hiyo umelipa heshima kubwa Bunge na Serikali na kwamba wana 
matarajio makubwa kwa sababu uwepo wake, utaliongezea Taifa ushirikiano 
na nchi nyingine za Afrika.
“Matarajio kwa Bunge ni makubwa 
kwani kuna mambo ambayo tunataka ushirikiano na nchi nyingine za 
Afrika, hivyo uwepo wako ni muhimu katika kufanikisha utekelezaji wake.”
Vilevile, Waziri Mkuu 
amewapongeza wabunge wengine wawili, Waheshimiwa David Silinde na Asha 
Abdullah Juma kwa ushirikiano wao uliochangia ushindi wa Mheshimiwa 
Masele.
Kwa upande wake, Mheshimiwa 
Masele ambaye ni Mbunge wa Shinyanga Mjini, ameishukuru Serikali kwa 
ushirikiano iliyompa na hatimaye kuibuka na ushindi huo.
Amesema ushindani ulikuwa mkali 
kutokana na uwepo wa mataifa mengi yaliyokuwa yakiwania nafasi hiyo. 
Aliahidi kutetea maslahi ya Taifa kwa muda wote atakaotumikia nafasi 
hiyo. “Nakuhakikishia Waziri Mkuu kwamba nitayalinda na kuyatetea 
maslahi ya Tanzania kwa muda wote ambao nitakuwa katika wadhifa huu,” 
alisema Mhe. Masele.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni