WAZIRI MKUU AMPONGEZA STEVEN MASELE


PMO_4427
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge Bungeni jijini Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
PMO_4467
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Kijitoupele Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha Bungeni jijini Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
PMO_4480
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenyeulemavu Jenista Mhagama, akijadili jambo na Waziri wa Elimu Profesa Joice Ndalichako, Bungeni jijini Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
PMO_4502
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Waziri wa Elimu Profesa Joice Ndalichako, Bungeni jijini Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_4546
PMO_4553
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika, Stephen Masele ambaye ni Mbunge wa Shinyanga Mjini, ofisini kwake Bungeni mjini Dodoma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
PMO_4567
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika, Stephen Masele ambaye ni Mbunge wa Shinyanga Mjini, ofisini kwake Bungeni mjini Dodoma, kutoka kushoto ni Mbunge wa Mbozi Magharibi Mheshimiwa David Silinde na Mbunge wa Viti Maalum Zanzibar Asha Abdullah Juma, Juni 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
PMO_4581 PMO_4584
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele na kumuahidi kwamba Serikali itampa ushirikiano ili aweze kutimiza majukumu yake.
Ametoa ahadi hiyo leo (Jumanne, Juni 5, 2018) wakati akizungumza na Mheshimiwa Masele ofisini kwake Bungeni, Dodoma. Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kumpongeza kwa kuchaguliwa kushika wadhifa huo.
Amesema ushindi wake katika nafasi hiyo umelipa heshima kubwa Bunge na Serikali na kwamba wana matarajio makubwa kwa sababu uwepo wake, utaliongezea Taifa ushirikiano na nchi nyingine za Afrika.
“Matarajio kwa Bunge ni makubwa kwani kuna mambo ambayo tunataka ushirikiano na nchi nyingine za Afrika, hivyo uwepo wako ni muhimu katika kufanikisha utekelezaji wake.”
Vilevile, Waziri Mkuu amewapongeza wabunge wengine wawili, Waheshimiwa David Silinde na Asha Abdullah Juma kwa ushirikiano wao uliochangia ushindi wa Mheshimiwa Masele.
Kwa upande wake, Mheshimiwa Masele ambaye ni Mbunge wa Shinyanga Mjini, ameishukuru Serikali kwa ushirikiano iliyompa na hatimaye kuibuka na ushindi huo.
Amesema ushindani ulikuwa mkali kutokana na uwepo wa mataifa mengi yaliyokuwa yakiwania nafasi hiyo. Aliahidi kutetea maslahi ya Taifa kwa muda wote atakaotumikia nafasi hiyo. “Nakuhakikishia Waziri Mkuu kwamba nitayalinda na kuyatetea maslahi ya Tanzania kwa muda wote ambao nitakuwa katika wadhifa huu,” alisema Mhe. Masele.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni