WAZIRI MKUU MGENI RASMI UZINDUZI WA KAMPENI YA UPIMAJI VVU JUNI 19 JIJINI DODOMA

Pix 01
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Leonald Maboko, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uzinduzi wa kampeni ya furaha ya yangu kuhamasisha huduma za kupima VVU na kuanza ARV mapema ambayo itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 19 jijini Dodoma.
Pix 02
Kaimu Mkurugenzi wa Kinga toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Angela Ramadhani akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu ya kuhamasisha huduma za kupima VVU na kuanza ARV mapema ambayo itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 19 jijini Dodoma..
Pix 03
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Leonald Maboko, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu kuhamasisha ya huduma za kupima VVU na kuanza ARV mapema ambayo itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 19 jijini Dodoma..
Pix 04
Baadhi ya washiriki wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Leonald Maboko (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu ya kuhamasisha huduma za kupima VVU na kuanza ARV mapema ambayo itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 19 jijini Dodoma..
Pix 05
Naibu Mkurugenzi wa Afya toka Shirika la Misaada la Marekani Bi. Ananthy Thambinayagan Ramadhani akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu ya kuhamasisha huduma za kupima VVU na kuanza ARV mapema ambayo itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 19 jijini Dodoma..
Picha na Eliphace Marwa – MAELEZO, Dar es Salaam.
…………….
NA WAMJW-DAR ES SALAAM 
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa,anatarajiwa kuzindua kampeni ya kitaifa ya Furaha yangu,mkoani Dodoma Juni 19 mwaka huu,inayohusisha upimaji wa VVU na kuanza kutumia ARV
Hayo yamezungumzwa na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya Dkt. Angera Ramadhan kuwa Kampeni hiyo imetajwa kuhamasisha mkakati wa serikali wa upimaji wa VVU na kuanza kutumia ARV mapema kwa wale watakaokutwa na maambukizi.

“Asilimia 45 ya wanaume wanajijua kuwa wanaishi na maambukizi ya VVU na asilimia 55 hawajijui huku wanawake waliokuwa wanajijua kuwa wanamaambukizi  ni asilimia 56 na 44 bado hawako tayari” alisema Dkt. Angera
Dkt. Angera amesema kuwa Kuanza ARV mapema kutapunguza wingi wa  VVU  mwilini na kuimarisha kinga kwa wagonjwa,hivyo kampeni hii kwa wanaume itakuwa chachu ya kujua afya zao na wengi kuwa tayari kwa kuimarisha afya na kupunguza hatari ya kuambukiza wenza wao. 
Aidha Dkt. Angera amesema kuwa serikali itaendelea kubuni mbinu mbadala ili kufikia malengo ya dira ya taifa ya kutokomeza maambukizi ya Ukimwi iliyoridhia malengo ya UNAIDS ya 90-90-90 ambayo ni kuhakikisha asilimia 90 ya watu wote wanaoishi na VVU  wanatambua afya zao,wanaanza dawa na kupunguza maambukizi mapya.
Naye Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI TACAIDS, Dkt. Leornad Maboko,alisema uzinduzi wa kampeni hiyo utakuwa na siku tano za kutoa huduma za afya bila malipo,ikiwemo upimaji wa VVU  na magonjwa sugu.
Aidha Dkt.  Maboko alisema kuwa  lengo la kuhamasisha kwa kauli ya Furaha yangu  Pima,Jitambur ,Ishi na mwanaume njoo kwenye huduma ni kutokana na kubaini kundi hilo kubwa halifikiwi na ili kumaliza maambukizi ni lazima kupewa hamasa.
“Hivyo tunatoa wito wakazi wa Dodoma,mikoa ya jirani na mikoa sita ambayo ipo katika awamu ya kwanza ya uzinduzi ikiwemo Njombe,Iringa na Mwanza kumuunga mkono Waziri Mkuu kwa kujitokeza kwa wingi kujua afya zao na ikigundulika kutumia dawa mapema ili kuiamrisha afya na kupunguza nguvu ya VVU,” alisema Dkt.  Maboko.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni