Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya 
Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Leonald Maboko, akifafanua 
jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uzinduzi wa 
kampeni ya furaha ya yangu kuhamasisha huduma za kupima VVU na kuanza 
ARV mapema ambayo itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 19 
jijini Dodoma.
 Kaimu Mkurugenzi wa Kinga toka 
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Angela
 Ramadhani akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu 
uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu ya kuhamasisha huduma za kupima VVU 
na kuanza ARV mapema ambayo itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim 
Majaliwa, Juni 19 jijini Dodoma..
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya 
Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Leonald Maboko, akifafanua 
jambo kwa waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu
 kuhamasisha ya huduma za kupima VVU na kuanza ARV mapema ambayo 
itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 19 jijini Dodoma..
Baadhi ya washiriki wakimsikiliza 
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. 
Leonald Maboko (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa kampeni ya furaha 
yangu ya kuhamasisha huduma za kupima VVU na kuanza ARV mapema ambayo 
itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 19 jijini Dodoma..
Naibu Mkurugenzi wa Afya toka 
Shirika la Misaada la Marekani Bi. Ananthy Thambinayagan Ramadhani 
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uzinduzi wa 
kampeni ya furaha yangu ya kuhamasisha huduma za kupima VVU na kuanza 
ARV mapema ambayo itazinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 19 
jijini Dodoma..
Picha na Eliphace Marwa – MAELEZO, Dar es Salaam.
…………….
NA WAMJW-DAR ES SALAAM 
WAZIRI Mkuu Kassim 
Majaliwa,anatarajiwa kuzindua kampeni ya kitaifa ya Furaha yangu,mkoani 
Dodoma Juni 19 mwaka huu,inayohusisha upimaji wa VVU na kuanza kutumia 
ARV
Hayo yamezungumzwa na Kaimu 
Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya Dkt. Angera Ramadhan kuwa Kampeni hiyo imetajwa kuhamasisha mkakati wa serikali wa upimaji wa
 VVU na kuanza kutumia ARV mapema kwa wale watakaokutwa na maambukizi.
“Asilimia 45 ya wanaume 
wanajijua kuwa wanaishi na maambukizi ya VVU na asilimia 55 hawajijui 
huku wanawake waliokuwa wanajijua kuwa wanamaambukizi  ni asilimia 56 na
 44 bado hawako tayari” alisema Dkt. Angera
Dkt. Angera amesema kuwa 
Kuanza ARV mapema kutapunguza wingi wa  VVU  mwilini na kuimarisha kinga
 kwa wagonjwa,hivyo kampeni hii kwa wanaume itakuwa chachu ya kujua afya
 zao na wengi kuwa tayari kwa kuimarisha afya na kupunguza hatari ya 
kuambukiza wenza wao. 
Aidha Dkt. Angera amesema kuwa
 serikali itaendelea kubuni mbinu mbadala ili kufikia malengo ya dira ya
 taifa ya kutokomeza maambukizi ya Ukimwi iliyoridhia malengo ya UNAIDS 
ya 90-90-90 ambayo ni kuhakikisha asilimia 90 ya watu wote wanaoishi na 
VVU  wanatambua afya zao,wanaanza dawa na kupunguza maambukizi mapya.
Naye Mkurugenzi wa Tume ya 
Kudhibiti UKIMWI TACAIDS, Dkt. Leornad Maboko,alisema uzinduzi wa 
kampeni hiyo utakuwa na siku tano za kutoa huduma za afya bila 
malipo,ikiwemo upimaji wa VVU  na magonjwa sugu.
Aidha Dkt.  Maboko alisema 
kuwa  lengo la kuhamasisha kwa kauli ya Furaha yangu  Pima,Jitambur 
,Ishi na mwanaume njoo kwenye huduma ni kutokana na kubaini kundi hilo 
kubwa halifikiwi na ili kumaliza maambukizi ni lazima kupewa hamasa.
“Hivyo tunatoa wito wakazi wa 
Dodoma,mikoa ya jirani na mikoa sita ambayo ipo katika awamu ya kwanza 
ya uzinduzi ikiwemo Njombe,Iringa na Mwanza kumuunga mkono Waziri Mkuu 
kwa kujitokeza kwa wingi kujua afya zao na ikigundulika kutumia dawa 
mapema ili kuiamrisha afya na kupunguza nguvu ya VVU,” alisema Dkt.  
Maboko. 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni