RC MAKONDA APOKEA SHEHENA YA VIFAA VYA MATIBABU KUTOKA KOREA KUSINI


IMG-20180627-WA0064
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo amepokea shehena ya Vifaa vya matibabu vyenye thamani ya shilingi milioni 100 kutoka serikali ya Korea Kusini kupitia shirika laKOICA.
IMG-20180627-WA0065
Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na Digital X-ray 3, Ultrasound 1, Kabati la usalama wa viumbe (safety cabinet) 1, Mashine 3 za kupima mkojo, mashine ya kuwapa joto watoto njiti (baby warmer) pamoja na mashine ya utakitshaji.
IMG-20180627-WA0067
Baada ya kupokea vifaa hivyo kutoka kwa Balozi wa Korea kusini Bwana Geum Young Song RC Makonda amekabidhi vifaa hivyo kwenye vituo vya Afya vya Sinza, Mnazi Mmoja na Mbagala ambako kuna uhaba wa vifaa. 
Kabla ya kupokea vifaa hivyo RC Makonda alifanya mazungumzo na Balozi huyo wa Korea kusini na kuwasilisha ombi la kujengwa kwa Chuo cha kisasa cha mafunzo ya udaktari na uuguzi ambapo Balozi Geum Young Song amepokea kwa mikono miwili ombi hilo.
IMG-20180627-WA0068
RC Makonda pia amemueleza Balozi ombi la kujengwa kwa kituo kikubwa cha upimaji wa magonjwa mbalimbali kwa wananchi kwenye eneo moja ambapo pia Balozi amepokea ombi hilo na kumsifu RC Makonda kwa moyo wake wa kujali wananchi. 
IMG-20180627-WA0069
Kwa upande wake Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania Bwana Geum Young Song amesema wametoa vifaa hivyo kuunga mkono kazi kubwa inayofanywa na Mkoa wa Dar es salaam katika uboreshaji wa sekta ya Afya na wataendelea kusaidiana na serikali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni