Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akitazama chombo cha kupima wingi wa mvua baada ya kuzindua vituo 51 vya
 kufuatilia  taarifa za hali ya hewa katika viwanja vya Ofisi ya 
Halmashauri ya wilaya ya Bahi mkoani Dodoma Juni 27, 2018.  Wengine 
pichani kutoka kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, 
Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu,Jenista Mhagama,Waziri wa 
Maji, Mhandisi Isaack Kamwele, Mwakilishi Mkaazi wa Mpango  wa Maendeleo
 wa Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bibi Natalie  Boucly na kulia ni 
Mbunge wa Viti Maalum kutoka mkoa wa Dodoma, Felista Bura.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa 
akizindua vituo 51 vya kufuatilia  taarifa za hali ya hewa katika 
viwanja vya Ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Bahi mkoani Dodoma Juni 
27, 2018.   Kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, 
Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama. Wanne kushoto ni 
Mwakilishi Mkaazi wa Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) 
nchini, Bibi Natalie Boucly.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akibonyeza kitufe wakati alipozindua vituo 51 vya kufuatilia  taarifa za
 hali ya hewa katika viwanja vya Ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Bahi 
mkoani Dodoma Juni 27, 2018.  K
ulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama
 Baadhi ya wananchi walioshiriki 
katika  uzinduzi wa vituo 51 vya kufuatilia  taarifa za hali ya hewa 
uliofanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika viwanja vya Ofisi ya 
Halmashauri ya wilaya ya Bahi mkoani Dodoma Juni 27, 2018.  
Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
………………..
WATAALAMU TUMIENI TAARIFA ZA TMA-MAJALIWA
WAZIRIMKUU Kassim Majaliwa 
amewataka wataalamu wa sekta za kilimo, mifugo na maji watumie taarifa 
za hali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) 
ili waongeze ufanisi katika utendaji kazi wao.
Ametoa agizo hilo leo 
(Jumatano, Juni 27, 2018) wakati akizinduavituo 51 vya kufuatilia 
taarifa za hali ya hewa, vituo 15 vya haidrolojia, kanzidata ya taarifa 
za hali ya hewa na kituo cha operesheni na mawasiliano ya 
dharura wilayani Bahi, Dodoma.
Amesemakuwa kuongezeka kwa 
vituo vipya vya kisasa vya ufuatiliaji wa mwenendo wa hali ya hewa 
kumeboresha uhakika wa utabiri kutoka asilimia 81 hadi 87 kama 
inavyoshuhudiwa kwenye taarifa zinazotolewa katika siku za hivi 
karibuni. “Hivi sasa tukiambiwa kwamba mvua itanyesha katika maeneo 
fulani tunakuwa na uhakika kwa asilimia 87 ya utabiri huo,”. 
“Vituo hivi ni muhimu katika 
kuimarisha uwezo wa nchi wa utoaji wa huduma za hali ya hewa na 
haidrolojia kwa ajili ya shughuli za maendeleo na kuongeza ufanisi 
katika utoaji wa tahadhari za awali za majanga yanayosababishwa na hali 
mbaya ya hewa na mabadiliko ya tabianchi,”. 
Amesema kupitia mradi huo 
uliofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) 
Serikali imeweza kufungua vituo 51 vya kisasa vya hali ya hewa katika 
maeneo mbalimbali nchini na vituo 15 vya kupima ujazo wa maji kwenye 
mito iliyopo kwenye mabonde ya Pangani, Ruvuma na Pwani ya Kusini 
ambavyo vinajiendesha vyenyewe. 
“Pia, mradi huu 
umeiwezesha Serikali kuanzisha kanzidata ya takwimu na taarifa za 
mafuriko         na ukame na taarifa za hali ya hewa na kuondoa 
ucheleweshwaji wa kupata takwimu au taarifa kutoka Wizara moja kwenda 
Wizara nyingine,” amesema. 
Hata hivyo, Waziri Mkuu 
ameziagiza Wizara ya Maji na Umwagiliaji na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi 
na Mawasiliano zitenge fedha kwenye bajeti zao ili ziweze kufuatilia na 
kusimamia mradi huo baada ya wafadhili kumaliza muda wao.
Waziri Mkuu amesema Serikali 
ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, itaendelea 
kushirikiana na washirika wa maendeleo katika kuhakikisha kuwa vituo na 
mifumo iliyowekwa inafanya kazi ipasavyo kwa usimamizi bora ili kufikia 
malengo yaliyokusudiwa.
Uzinduzi huo umehudhuriwa na 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Vijana, Kazi, Ajira 
na Wenye Ulemavu, Bibi Jenista Mhagama, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, 
Mhandisi Isack Kamwelwe na Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba.
Wengine ni Naibu Waziri wa 
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, Naibu 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Kangi 
Lugola, Wabunge na Mwakilishi Mkaazi wa Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa 
Mataifa (UNDP) nchini Bibi Natalie Boucly.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni