Na Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma
Benki 
ya NMB imetoa gawio la Sh. bilioni 10.1 kwa Serikali ambayo inamiliki 
asilimia 32 ya hisa za Benki hiyo baada ya kupata faida ya Sh. bilioni 
94.8 baada ya kodi kwa mwaka 2017/2018.
Tukio 
hilo la kukabidhi hundi kifani ya gawio hilo limefanyika Makao Makuu ya 
Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dodoma, kati ya Waziri wa Fedha na 
Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango, kwa niaba ya Serikali, na Mkurugenzi 
Mtendaji wa Benki hiyo Ineke Bussemaker. 
Dkt. 
Mpango amezipongeza juhudi za watendaji wa Benki hiyo waliofanikisha 
kupatikana kwa faida iliyowezesha Serikali kupata gawio licha ya 
changamoto zilizoikumba Sekta ya Benki likiwemo suala la mikopo 
chechefu.
“Mikopo
 chechefu imekua tatizo kwa Benki nyingi nchini hivyo ninatoa rai kwa 
Benki ya NMB kuhakikisha inafuata taratibu za kukopesha na kuendelea 
kusimamia vizuri wakopaji ili kuondoa tatizo la mikopo chechefu” 
alieleza Dkt. Mpango. 
Aidha 
ameipongeza Benki hiyo kwa kutoa huduma katika Sekta ya kilimo na 
kuitaka ipanue wigo zaidi na kuziwezesha sekta za uvuvi na ufugaji 
kutokana na umuhimu wake katika ukuaji wa uchumi wa taifa. 
Alisema
 kuwa anatarajia Benki hiyo itatoa gawio zaidi mwaka ujao wa fedha na 
amemwagiza Msajili wa Hazina, kuzihakiki taasisi zote ambazo Serikali 
imewekeza hisa zake ili zitoe gawio lasivyo ametishia Serikali kuondoa 
hisa zake kwakuwa uwekezaji huo hautakuwa na tija. 
Kwa 
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Ineke Bussemaker alieleza 
kuwa licha ya Benki yake kutoa gawio hilo la shilingi bilioni 10.1 kwa 
Serikali, pia inalipa kodi za Serikali vizuri ambapo katika kipindi cha 
mwaka 2017/18 imetoa kodi ya shilingi bilioni 127.
Aliongeza
 kuwa tangu mwaka 2014 hadi 2017 benki hiyo imetoa kodi zinazofikia 
zaidi ya shilingi bilioni 460 na kwamba itaendelea kuongeza ufanisi wa 
utoaji wa huduma za kibenki ili iweze kupata faida na kulipa gawio kubwa
 zaidi kwa wana hisa wake ikiwemo Serikali inayomiliki silimia 31.8 ya 
hisa 500.
Aidha,
 amesema kuwa Benki yake imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Sekta ya 
Kilimo kwa kutoa huduma za kifedha kwa wakulima wakiwemo wakulima wa 
Tumbaku na Korosho katika mikoa ya Kusini ya Lindi na Mtwara, ambapo 
imefungua zaidi ya akaunti 300,000 na kuweza kukusanya zaidi ya shilingi
 bilioni 250 mwezi Novemba mwaka jana.
Bi. 
Bussemaker alisema kuwa Benki yake inajitahidi kuhakikisha kunakua na 
huduma jumuishi za kifedha kwa wananchi kote nchini kwa kuweka Mawakala 
na kuongeza Matawi ya Benki hiyo na pia kuhamasisha wananchi wafungue 
Akaunti ya Benki hiyo.
Alisema
 kuwa ili kufanikisha utoaji wa huduma hiyo ya kifedha kwa watanzania, 
Benki hiyo imejipanga kutumia teknolojia ya kisasa ya masuala ya fedha 
ambayo itarahisisha kuwafikia watu wengi ikiwemo huduma za fedha kwa 
njia ya simu za mkononi. 
Katika
 Mwaka wa Fedha 2016/2017, Benki hiyo ilitoa gawio la shilingi bilioni 
16.5 kwa Serikali, huku kukiwa na pungufu ya shilingi bilioni 6 mwaka 
huu hatua iliyomlazimu Dkt. Mpango kuiagiza Benki hiyi ihakikishe 
inaboresha huduma zake ili Serikali ipate gawio kubwa zaidi kwa ajili ya
 kutumia fedha hizo kuwaletea wananchi maendeleo katika sekta za maji, 
afya, elimu, na miundombinu mingine muhimu.
 Mkurugenzi
 Mtendaji wa Benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker (kulia), akieleza kuhusu 
mkakati wa Benki yake wa kuhakikisha inaongeza ufanisi na kufungua 
akaunti za wateja wengi zaidi, wakati wa hafla ya kutoa gawio la Sh. 
bilioni 10.1 kwa Serikali ambayo ni mwanahisa, katika ukumbi wa Wizara 
ya Fedha na Mipango Jijini Dodoma.
 Msajili
 wa Hazina Bw. Athuman Mbuttuka (Kushoto), Kaimu Kamisha wa Sera wa 
Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Benedict Mgonya (katikati) na Kamishna wa
 Fedha za Nje wa Wizara hiyo Bw. John Rubuga, wakisikiliza kwa makini 
maelezo ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor. Mpango 
(Mb), kuhusu taasisi za fedha kutakiwa kuwafikia wafugaji na wavuvi 
wakati wa kupokea gawio la Sh. bilioni 10.1 kutoka Benki ya NMB, Jijini 
Dodoma.
 Kaimu
 Kamishna wa Sera Bw. William Mhoja (kushoto) na Kamishna Msaidizi wa 
Bajeti Bw. Pius Mponzi, wakifuatilia tukio la Benki ya NMB kuipatia 
Serikali inayomiliki asilimia 32 ya hisa za Benki hiyo, mgao wa Shilingi
 bilioni 10.1, baada ya kupata faida katika biashara mwaka 2017.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor. Mpango (Mb) (mbele),  akitoa maelekezo kwa taasisi za fedha kuzingatia kanuni za kukopesha ili kuondoa mikopo chechefu,  wakati
 wa hafla ya Benki ya NMB kutoa gawio la Sh. bilioni 10.1 kwa Serikali 
ambayo ni mwanahisa, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini 
Dodoma.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor. Mpango (Mb),  akitoa
 maelekezo kwa Msajili wa Hazina, Bw. Athuman Mbuttuka, kuzihakiki 
taasisi zote ambazo Serikali imewekeza hisa zake ili zitoe gawio kwa 
Serikali, wakati wa hafla ya Benki ya NMB kutoa gawio la Sh. bilioni 
10.1 kwa Serikali ambayo ni mwanahisa, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha 
na Mipango, Jijini Dodoma.
 Waziri
 wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor. Mpango (Mb) (wa sita 
kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker (wa 
saba kushoto) na Maafisa waandamizi kutoka Benki ya NMB na Wizara hiyo 
wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Serikali kupokea gawio la Sh. 
bilioni 10.1 kutoka NMB, Jijini Dodoma.
 Waziri
 wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor. Mpango (Mb) (kushoto) 
akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Bi. Ineke 
Bussemaker, baada ya kupokea gawio la Sh. bilioni 10.1 kutoka NMB, 
katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dodoma.
 Waziri
 wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor. Mpango (Mb) (kushoto) na 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker, wakiangalia 
hundi kifani yenye thamani ya shilingi bilioni 10.1, ambayo ni gawio 
lililotolewa na Benki ya NMB kwa Serikali, Jijini Dodoma.
Waziri
 wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor. Mpango (Mb) (kushoto) na 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker, wakipeana 
mkono wakati wa makabidhiano ya hundi kifani yenye thamani ya shilingi 
bilioni 10.1, ambayo ni gawio lililotolewa na Benki ya NMB kwa Serikali,
 Jijini Dodoma.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni