mkurugenzi wa uchaguzi akiwa anatangaza matokeo ya
ubunge na urais wa jimbo la arumeru magharikibi
ubunge na urais wa jimbo la arumeru magharikibi
 picha ikionyesha wananchi  na waandishi wa habari wakiwa wanaangalia
matokeo ya ubunge na urais yaliyobandikwa kwenye ubao wa matangazo
katika jimbo la Arumeru magharib
matokeo ya ubunge na urais yaliyobandikwa kwenye ubao wa matangazo
katika jimbo la Arumeru magharib
 mgombea ubunge wa jimbo la Arumeru magharibi akiwa
makini kusikiliza matokeo ya urais na ubunge ya jimbo lake wakati
mkurugenzi wa halmashauri ya meru ambaye pia msimamizi wa uchaguzi
wa jimbo hilo Fidelis Lumato
Na Mahmoud Ahmadmakini kusikiliza matokeo ya urais na ubunge ya jimbo lake wakati
mkurugenzi wa halmashauri ya meru ambaye pia msimamizi wa uchaguzi
wa jimbo hilo Fidelis Lumato
Mbunge wa jimbo la Arumeru magharibi Olemeiseyeki
Gibson  Blasius  amewashukuru wananchi wa jimbo lake kwakuweza
kumchagua kuongoza jimbo hilo  na
amewahidi kutofanya mchezo katika kipindi cha uongozi wake.
Ameyasema hayo leo mara baada ya kutangazwa  kuwa mshindi wa jimbo hilo baada
yakuongoza   kwa kura nyingi zaidi ya
wenzake.
Alisema kuwa anawashukuru wananchi wa jimbo hilo kwa kumpa
kura nakumchagua kwani hii wamemuona ni kiongozi  anaeyefaa kuwaongoza na ni kiongozi
mchapakazi.
Adha aliwashukuru wananchi wa jimbo hilo kwa kuweza kumpa madiwani
wengi zaidi  katika halmashauri yake na
kusema kuwa  kati ya kata 27 zilizopo
jimboni kwake  jumla ya kata 21 ni za
chadema  na zingine 6 niza CCM
Kwa mujibu  wa taarifa
iliyotolewa  na mkurugenzi wa
Halmashauri  ya meru ambaye pia ni
msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Arumeru magharibi wakati akitangaza matokeo  matokeo ya nafasi ya urasi katika jimbo hilo
Fidelis Lumato  alianza na chama cha Act
ambapo waliweza kupata kura 324  ,ADC 250
,CCM27658,CDM 105720,CHAUMA 388,NRA58,TLP54 pamoja na UPDP 40.
Kwa upande  wa jimbo
la Arumeru magharibi  mgombea huyu wa
ubunge kupitia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Olemeiseyeki
Gibson  Blasius  ameweza kuongoza  kwa asilimia 73% ambapo alipata  kura 94354 
huku mgombea aliyemfuata ni wa chama cha mapinduzi( CCM)Sabaya  Loy Thomas  ambaye alipata kwa asilimia 25%  ambapo alipata kura 32831 huku chama cha ACT
Wilson Loilole Laizer kikiwa kimepata kura kwa asilimia 2% ambapo walipata kura
2457.
Lumato alisema kuwa anapenda kuwashukuru wananchi pamoja na
wagombea kwa jinsi walivyoonyesha  hali
ya utulivu katika kipindi chote cha kampeni pamoja,upiga kura pamoja na kupokea
matokeo na amewaomba waendelee hivyo hivyo hata katika chaguzi zijazo.
Afafanua kwanini wamechelewa kutaja matokeo na kusema kuwa
hii imetokana na tatizo la mtandao ambapo lilitokea tangu hali iliyowapelekea  kuchelewesha matokeo hadi leo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni