DSC_4474
Makamu wa Rais wa Zimbabwe, Mh. Emmerson Mnangagwa  akihutubia wakati wa ufunguzi rasmi wa mkutano wa tano wa  Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo endelevu barani Afrika  unaoendelea muda huu Victoria Falls-Zimbabwe. Ambapo amezitaka nchi za Afrika kuendelea kushikamana katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na ukuaji wa uchumi. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog)
DSC_4488
Baadhi ya washiriki wa mkutano mkubwa wa tano wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo endelevu barani Afrika unaoendelea muda huu Victoria Falls-Zimbabwe wakifuatilia mada mbalimbali kwa watoa mada (hawapo pichani). Mada mbalimbali za kujadili juu ya Afrika hatua ya kuchukua kuelekea mkutano mkubwa wa Dunia wa COP 21, utakaofanyika nchini Paris, Ufaransa mwishoni mwa mwaka huu. 
Na Andrew Chale, Modewjiblog
[VICTORIA FALLS-ZIMBABWE] Mkutano mkubwa  wa tano wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo endelevu barani Afrika umeanza rasmi leo katika mji wa Kitalii wa Victoria Falls, Nchini hapa huku ukishirikisha watu mbalimbali kutoka nchi za Afrika na nje ya Afrika.
Washiriki wanaoshiriki mkutano huu unaondelea hapa ni pamoja na wadau wa mambo ya mazingira, wanaharakati, taasisi binafsi, Serikali, Mashirika ya kijamii, Wafanyabiashara, wanahabari na viongozi wa Kiserikali na wanasiasa katika kujadili kwa pamoja.
Mkutano huo umeanza rasmi leo Oktoba 28-30, wiki hii umeandaliwa  kwa ushirikiano wa mashirika mbalimbali ikiwemo UNECA, Serikali ya Zimbabwe pamoja na mashirika mengineyo.
DSC_4482
DSC_4478
DSC_4490
DSC_4424
DSC_4434
DSC_4485