Makamu wa Rais wa Zimbabwe, Mh. Emmerson Mnangagwa  akihutubia wakati wa ufunguzi rasmi wa mkutano wa tano
 wa  Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo endelevu barani Afrika 
 unaoendelea muda huu Victoria Falls-Zimbabwe. Ambapo amezitaka nchi za 
Afrika kuendelea kushikamana katika kukabiliana na mabadiliko ya 
tabianchi pamoja na ukuaji wa uchumi. (Picha zote na Andrew Chale, 
Modewjiblog)
Baadhi
 ya washiriki wa mkutano mkubwa wa tano wa Mabadiliko ya Tabianchi na 
Maendeleo endelevu barani Afrika unaoendelea muda huu Victoria 
Falls-Zimbabwe wakifuatilia mada mbalimbali kwa watoa mada (hawapo 
pichani). Mada mbalimbali za kujadili juu ya Afrika hatua ya kuchukua 
kuelekea mkutano mkubwa wa Dunia wa COP 21, utakaofanyika nchini Paris, 
Ufaransa mwishoni mwa mwaka huu. 
Na Andrew Chale, Modewjiblog
[VICTORIA
 FALLS-ZIMBABWE] Mkutano mkubwa  wa tano wa Mabadiliko ya Tabianchi na 
Maendeleo endelevu barani Afrika umeanza rasmi leo katika mji wa Kitalii
 wa Victoria Falls, Nchini hapa huku ukishirikisha watu mbalimbali 
kutoka nchi za Afrika na nje ya Afrika.
Washiriki
 wanaoshiriki mkutano huu unaondelea hapa ni pamoja na wadau wa mambo ya
 mazingira, wanaharakati, taasisi binafsi, Serikali, Mashirika ya 
kijamii, Wafanyabiashara, wanahabari na viongozi wa Kiserikali na 
wanasiasa katika kujadili kwa pamoja.
Mkutano
 huo umeanza rasmi leo Oktoba 28-30, wiki hii umeandaliwa  kwa 
ushirikiano wa mashirika mbalimbali ikiwemo UNECA, Serikali ya Zimbabwe 
pamoja na mashirika mengineyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni