WAZIRI
 MKUU Mizengo Pinda amesema hajahama Chama cha Mapinduzi (CCM) kama 
ambavyo imekuwa ikidaiwa na baadhi watu na mitandao ya kijamii kwamba 
amejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
 
 
Alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti jana (Jumamosi,
 Oktoba 24, 2015) na wakazi wa majimbo ya Mpanda Mjini na Kavuu kwenye 
mikutano minne ya hadhara iliyofanyika katika kata za Kakese, Kibaoni, 
Usevya na Majimoto wakati akifunga kampeni za uchaguzi mkoani Katavi.
 
 “Kuna picha zimesambaa mitandaoni zinadai nimehamia CHADEMA. Hivi 
kweli, sasa hivi nahamia huko ili iwe nini?” Alihoji na kushangiliwa na 
wakazi wa majimbo hayo.
 
 Alisema picha wanazozisambaza ni za mwaka 2012 ambazo zilipigwa wakati
 akionyesha kwa wananchi moja ya kadi alizopokea kutoka kwa wanachama
 wa CHADEMA.
 
 Katika moja ya picha hizo, Waziri Mkuu Pinda anaonekana akiwa na mlinzi
 wake huku akionyesha kadi ya CHADEMA. Hakuna kiongozi yeyote wa CHADEMA
 anayeonekana akimkabidhi kadi kama mwanachama mpya.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni