WAASI WA COLOMBIA WAVAMIA KUNDI LA WATU NA KUWAUA 12


Waasi wenye kufuata mrengo wa kushoto nchini Colombia wamevamia kundi lililokuwa limebeba kura na kuuwa watu 12, vikosi vya usalama vya nchi hiyo vimeeleza.

Waziri wa Ulinzi Luis Carlos Villegas amesema kundi hilo la mrengo wa kushoto katika eneo la kaskazini mwa Guican, lilifanya shambulio hilo.

Amesema kundi la Jeshi la Taifa la Ukombozi wa Colombia ambalo ni kundi kubwa la waasi nchini humo ndilo lililotekeleza shambulizi hilo. Rais Juan Manuel Santos ameahidi kujibu mapigo ya tukio hilo dhidi ya waasi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni