ZAIDI YA WASTAAFU 40 WAFA KATIKA AJALI YA BASI ILIYOTOKEA NCHINI UFARANSA

Zaidi ya wastaafu 40 waliokuwa kwenye safari fupi wamekufa katika ajali ya basi lililogongana na lori katika barabara kusini mashariki mwa Ufaransa.

Ajali hiyo imetokea karibu na Puisseguin katika mkoa wa Gironde mashariki mwa Bordeaux, ikiwa si mbali tangu basi hilo lilipoanza safari yake katika mji uliokaribu.

Rais wa Ufaransa Francois Hollande ametuma twitti akisema serikali imeguswa mno na tukio hilo la ajali hiyo mbaya.

Hii ni ajali mbaya ya barabarani kutokea nchini Ufaransa tangu mwaka 1982 ambayo iliuwa watu 52.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni