Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu (Pichani) amesema kuwa maandalizi kwa ajili ya shughuli ya kufunga kampeni za Uchaguzi Mkuu kitaifa kwa upande wa Chama hicho inayotarajiwa kufanyika hii leo katika Uwanja wa CCM Kirumba yamekamilika.
                                                                                                   Na:George Binagi-GB 
Pazzo kubwa
 itafungwa nje ya uwanja huo kwa ajili ya wale watakaokosa nafasi ya 
kuingia uwanjani kwa kuwa shughuli hiyo inatarajiwa kuhudhuriwa na 
maelfu ya wakazi wa Jiji la Mwanza na Maeneo jirani.
Mbali na 
Mgombea Urais wa CCM Dkt.John Pombe Magufuli kuwepo katika mkutano huo, 
pia Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
anaemaliza muda wake Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuwa miongoni
 mwa viongozi watakaohudhuria katika Mkutano huo wa Ufungaji wa Kampeni 
za Uchaguzi Mkuu kwa upande wa CCM.
Wakati 
Watanzania wakitarajia kushiriki zoezi la Uchaguzi Mkuu siku ya kesho 
jumapili ya Octoba 25, Chama cha Mapinduzi CCM kimejihakikishia ushindi 
mnono katika maeneo mbalimbali nchini kuanzia ngazi ya udiwani, Ubunge 
na Urais.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni