MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO, AMOS MAKALLA AKUTANA NA MAOFISA WA JESHI LA POLISI MJINI MOSHI, PIA ATEMBELEA GEREZA KUU LA KARANGA

Maofisa mbalimbali wa jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro wakimsikiliza Mkuu wa mkoa huo, Mh Amos Makalla ( hayupo pichani ) wakati alipokutana na kuzungumza nao.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mh Amos Makalla ( katikati ) akiwa na viongozi wakuu wa jeshi la polisi mkoani humo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mh Amos Makalla akizungumza na maofisa mbalimbali wa jeshi la polisi mkoani humo.

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mh Amos Makalla amezungumza na polisi wa Manispaa ya Moshi na kuwataka wahakikishe uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu ili kila Mwananchi apate haki ya kupiga kura bila kubughudhiwa.

Amewataka polisi kuhakikisha kuanzia sasa, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi wahakikishe amani inatawala na katika kutekeleza majukumu yao wazingatie maadili ya polisi.

Aidha akiwa katika gereza la Karanga, mkuu huyo wa mkoa wa Kilimanjaro amekagua malazi ya wafungwa na mahabusu, na baadaye  akaongea na baraza la Askari na kukagua kiwanda cha viatu na ushonaji unaofanywa na wafungwa na mahabusu

Amepongeza ubora wa viatu vinavyotengenezwa kiwandani hapo na bidhaa za ushonaji unaofanywa na gereza ka wanawake

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mh Amos Makalla akisalimiana na maofisa wa jeshi la Magereza alipotembelea gereza la Kuu la Karanga lililopo nje kidogo ya mji wa Moshi.
Maofisa wa jeshi la Magreza wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mh Amos Makalla ( hayupo pichani ) wakati alipokutana na kuzungumza nao.
Maofisa wa Magereza wakimtembeza mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mh Amos Makalla ( mwenye kaunda suti ya kaki ) alipotembelea gereza kuu la Karanga lililopo nje kidogo ya mji wa Moshi.
                                                                                                       Picha ya pamoja
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mh Amos Makalla akikagua viatu vinavyotengenezwa na wafungwa wanaotumikia vifungo vyao katika gereza kuu la Karanga.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni