JITIHADA ZA UOKOAJI ZINAIMARIKA KUSAIDIA WATU WALIOATHIRIKA NA TETEMEKO

Jitihada za uokoaji zinaimarika kusaidia watu walioathirika na tetemeko lenye kipimo cha alama 7.5 lililolikumba eneo la kando la Afghanistan na Pakistan hapo jana.

Watu wapatao 275 inasemekana wamekufa na zaidi ya 2,000 wamejeruhiwa. Timu ya uokoaji imetumwa katika mlima ulio eneo le kando ambako madhara ya tetemeko hayajajulikana.

Miongoni mwa waliopoteza maisha ni pamoja na wanafunzi wa kike nchini Afghanistan ambao walikufa kwa kukanyagana wakati wakijaribu kutoka kwenye jengo lililoanguka.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni