KIJANA ALIYEUA MWALIMU NA MWANAFUNZI SWEDEN NI MBAGUZI

Kijana aliyefunika uso wake ambaye alimuua mwalimu na mwanafunzi katika shule nchini Sweden, alisukumwa na dhamira ya ubaguzi.

Mkuu wa polisi Niclas Hallgren amesema wamebaini hilo baada ya kukuta ushahidi kwenye makazi ya muuaji huyo, unaoelezea mwenendo wa matendo yake.

Vyombo vya habari vimeripoti kuwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 21, alikuwa ni mfuasi wa kundi lenye kufuata msimamo wa mrengo wa kulia.

Kijana huyo aliyekuwa amevaa kofia ya pikipiki na kufunika uso wake akiwa na jambia alivamia shule hiyo eneo la Trollhattan karibu na Gothenburg, kabla ya kupigwa risasi na kufa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni