POLISI NCHINI MEXICO WAMEBAINI NJIA YA SHIMO LA ARIDHINI YENYE UREFU WA MITA 800

Polisi nchini Mexico wamebaini njia ya shimo la aridhini yenye urefu wa mita 800, inayotumika kusafirishia dawa za kulevya kwenda Mji wa San Diego nchini Marekani.

Shimo hilo linaloanzia katika mji wa Tijuana nchini Mexico, linasemekana ni la mkuu wa genge la dawa za kulevya anayetafutwa Joaquin Guzman.

Polisi nchini Mexico wamesema wanawashikilia watu 16, na wamekamata tani 10 za bangi.

Wauza dawa za kulevya nchini Mexico wamekuwa wakisafirishwa kwa njia za magendo dawa za kulevya kwenda Marekani kupitia njia za mashimo ya aridhini.
                                Polisi akilinda shehena ya dawa za kulevya iliyokamatwa

You might also like:

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni