ANGELINA JOLIE LICHA YA KUWA MIONGONI MWA NYOTA MKUBWA HATAKI MATANUZI

Nyota wa filamu Angelina Jolie licha ya kuwa miongoni mwa nyota wakubwa kabisa duniani lakini anapenda kuishi maisha ya kawaida badala ya yale ya udiva.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 40, ameonekana akiwasili katika uwanja wa ndege wa LAX akivuta mwenywe begi lake la matairi bila ya kuwa na msaidizi kama wafanyavyo mastaa wengine, akiwa na watoto wake.

Angelina Jolie alikuwa na watoto wake hao Maddox, Pax, Zahara pamoja na Shiloh, ambao nao walikuwa wamebeba mabegi yao mgongoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni