CHAMA CHA CONSERVATIVE CHA SHERIA NA HAKI KIMESHINDA UCHAGUZI POLAND

Chama cha Conservative cha Sheria na Haki kimeshinda uchaguzi wa bunge nchini Poland.

Kura za mwisho zinaonyesha chama hicho kimepata viti vingi kuweza kutawala peke yake, huku ikitarajiwa kupata kura asilimia 39.

Kiongozi wao Jaroslaw Kaczynski amedaia kupata ushindi, huku waziri mkuu anayeondoka Ewa Kopacz wa chama cha mrengo wa kati cha Civic Platform akikubali kushindwa.

Chama cha Sheria na haki kinaungwa mkono mno katika maeneo ya vijijini nchini Poland.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni