MTN NIGERIA YAPIGWA FAINI ILIYOWEKA REKODI YA DOLA BILIONI 5.2

Kampuni kubwa ya simu ya MTN nchini Nigeria imepigwa faini iliyoweka rekodi ya dola bilioni 5.2 na Tume ya Mawasiliano ya Nigeria (NCC).

MTN wamepigwa faini hiyo kwa kushindwa kutimiza kwa muda masharti ya NCC ya kuwafutia mawasiliano watumiaji wa simu ambao hawajasajili kadi zao za simu.

Kampuni ya MTN Nigeria imesema itapitia barua ya faini hiyo walioyowasilishwa na Tume ya Mawasiliano ya Nigeria (NCC).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni