MAMA SAMIA NA DK. SHEIN WAFUNGA KAZI MKUTAO WA KUFUNGA KAMPENI ZA CCM ZANZIBAR

Maelfu ya wananchi wakiwa wamefurika kwenye Viwanja vya Kibandamaiti, wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za CCM, uliofanyika leo kwenye Viwanja hivyo mjini Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk. Ali Mohammed Shein akisalimiana na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu hassan baada ya kuwasili kwenye mkutano wa kufunga kampeni za CCM uliofanyika leo kwenye Viwanja vya Kibandamaiti mjini Zanzibar.
Mgombea wa Urais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein akimsalimia Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za CCM uliofanyika kwenye Viwanja vya Kibandamaiti mjini Zanzibar leo. Wengine ni Makamu wa Rais Dk. Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi na Waziri Kiongozi Mstaafu, Shamsi Vuai Nahodha
Mgombea Mwenza Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk. Ali Mohamed Shein, katika mkutano wa kufunga kampeni za CCM uliofanyika leo katika viwanja vya Kibanda maiti mjini Zanzibar

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni