NYUMBA
 ya Naibu sheha wa shehia ya Tibirinzi wilaya ya Chake chake Pemba, 
Bikombo Simai Juma (42), ambayo imedaiwa kuchomwa moto na watu 
wasiofahamika kwa madai ya hitilafu za kisiasa, tukio hilo lilitokea 
oktoba 26, majira ya saa 7:00 usiku, ambapo wakati huo alikuwa ndani 
amelala na jumla ya watu 13 akiwemo mtoto mchanga wa mwezi mmoja, 
walisalimika kufa, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
NYUMBA
 nyengine ilioko kando mwa nyumba ya naibu sheha, eneo hilo la 
Tibirinzi, kijiji cha Minazini, ikiwa imechomwa moto nyuma kwenye eneo 
la choo cha makuti, inayomilikiwa na Khamis Kassim Juma siku hiyo hiyo 
ya Oktoba 26 usiku wa saa 7:00 ambapo matukio yote hayo hakuna 
aliejeruhiwa, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
NAIBU
 sheha wa shehia ya Tibirinzi wilaya ya Chake chake Pemba Bikombo Simai 
Juma (24) akizungumza na mwandishi wa habari hizi hayupo pichani, muda 
mfupi baada ya nyumba yake kudai kutiliwa moto na watu wasiofahamika, 
(Picha na Haji Nassor, Pemba). Kwa hisani ya ZanziNews
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni