WATU 27 WARIPOTIWA KUWA NA UGONJWA KIPINDU PINDU JIJINI ARUSHA

index 
 Mahmoud Ahmad Arusha
Jumla ya watu 27 waliripotiwa kuwa na dalili za ugonjwa wa kipindupindu huku kati yao 6 walithibitishwa kuwa na ugonjwa wa kipindupindu. Na watano wamelazwa katika kituo cha Afya Levolosi.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake mkuu wa wilaya ya Arusha Fadhili Nkurlu aliwataka wakazi wa jiji la Arusha kufuata kanuni za ugonjwa huo na kuwa waepuke kula vyakula sehemu zisizofaa.

Nkurlu alisema kuwa kwa zaidi ya miezi miwili sasa maeneo mbali mbali hapa nchini yameripitiwa kuwa na ugonjwa huo katika mikoa ya Dar es salaam.Morogoro,Pwani na mkoa wa Jirani wa Kilimanjaro mnamo mwezi wa nane mwaka huu.

Alisema kuwa aidha katika siku za hivi karibuni mikoa ya Singida na Shinyanga nayo iliripotiwa kuwa na ugonjwa huo na mgonjwa wa kwanza kuripotiwa mkoani hapa ni kutoka mkoani Sngida na alilazwa na kupatiwa matibabu na kuruhusiwa kwa kuanza kutapika na kuharisha akiwa njiani kuja Arusha.

Alitanabaisha kuwa wagonjwa walioripotiwa wanatoka katika Mkoa wa Singida watatu,mmoja anatoka halmashauri ya Arusha dc,mmoja kutoka halmashauri ya Simanjiro na wagonjwa 22 wanatokea hapa jijini Arusha,

“Nawasihi wakazi wa jiji la Arusha kutambua kuwa ugonjwa wa Kipindupindu umeingia hapa jijini kwetu na hivyo mfuate maagizo ya wataalamu wa Afya kuepuka kula vyakula visivyochemshwa na vilivyo kwenye mazingira machafu kuepuka kupata maambukizi ya ugonjwa wa kipindu pindu”alisema Nkurlu’

Pamoja na ukweli kwamba ugonjwa wa kipindupindu unatibika hasa mgonjwa anapowahi matibabu pia inashauriwa wananchi ni vizuri kujikinga na ugonjwa huo kwa njia za upatikanaji wa maji safi na salama na kunywa maji aliyochemshwa pia kunawa mikono baada ya kutoka msalani,
Mwisho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni