NCHI YA CONGO-BRAZZAVILLE KUFANYA UPIGAJI KURA YA MAONI CONGO-BRAZZAVILLE

Nchi ya Congo-Brazzaville inafanya upigaji kura ya maoni kuhusiana na kubadilishwa Katiba katika kumruhusu rais Denis Sassou Nguesso kugombea kwa muhula wa tatu.

Viongozi wa upinzani wametaka kususiwa kwa kura hiyo baada ya idadi kadhaa ya waandamanaji kupigana na maafisa wa ulinzi.

Chini ya Katiba ya sasa, rais Nguesso hawezi kuwania urais kutokana na kuwa na umri zaidi ya miaka 70, na tayari ametumikia mihula miwili. Rais Sassou Nguesso aliingia madarakani mwaka 1979.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni