Leo
 saa 3 na dakika 25 Usiku mkuu wa wilaya Mh Richard Kasesela alipokea 
wakina mama 3 wakiwa wanatetemeka kwa baridi, wakilalamika kumwagiwa 
maji walipokuwa wamekaa kwenye eneo la kusubiria wagonjwa walio lazwa 
hasa kwa wale walio toka mbali.  
Maji hayo yalimwagwa na walinzi wa kampuni ya Amazon ambao ndio wamepewa kandarasi ya ulinzi hospitali ya Rufaa ya Iringa.
 Mkuu
 wa wilaya Iringa, Richard Kasesela alifika hospitali kujionea mwenyewe 
hali halisi, baadae pia akapata taarifa kuwa jana yake Mlinzi alimpiga 
mzee aliyekuwa ameleta chakula hospitali na kumwaga kwa mateke.  
Mkuu wa wilaya aliamuru mlinzi huyo na mwenzake wakamatwe pia mwenye kampuni afike kituo cha polisi haraka iwezekanavyo. 
"Hali
 hii imeudhi sana hasa ukiona jinsi wakina mama walivyo nyanyasika 
wengine vyombo vyao na chakula kuroweshwa maji." alisema Mh Kasesela. 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni