RUBANI WA NDEGE ILIYOANGUKA JUU YA MTI ALALA USIKU MZIMA JUU YA MTI

Rubani wa ndege ndogo iliyoanguka juu ya mti amelazimika kulala usiku juu ya mti na kusubiri kwa saa 12 baada ya waokoaji kusema inabidi wasubiri hadi pakuchwe ili wamuokoe.

Rubani na ndege hiyo ilianguka na kutua juu ya mti, karibu kilomita 30 mashariki mwa Mji wa Stuttgart kusini mwa Ujerumani jumatatu usiku.

Waokoaji walihofia kufanya zoezi la uokoaji usiku wa manane kwa kuogopa kuwa wakifanya hivyo huenda ndege hiyo ikaanguka chini ya mti.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni