UVCCM KUINGIA MIKATABA MIPYA NA WAPANGAJI WAKE



Image result for NEMBO YA UVCCMNa Mahmoud Ahmad Arusha

Katibu wa Uvccm mkoa wa Arusha Ezekiel Mollel amesema kuwa umoja huo utaendelea na kuingia mikataba mipya na wapangaji wake waliondani ya vibanda na si vingine.


Kauli hiyo ameitoa leo wakati akiongea na wanahabari ofisini kwake ambapo alikumbushia siku 14 walizotoa kwa wapangaji hao wa umoja huo wa vijana kuwa zimeisha na yeyote atakaekadi hatua zitachuliwa.


Mollel alisema kimsingi wamekubaliana kuingia mkataba mipya na wapangaji wote kwenye vibanda 49 vinavyomilikiwa na umoja huo kwa wapangaji  kuingia mkataba wa mwaka mmoja mmoja.


Akatanabaisha kuwa na wale wapangaji waliowapangishia hapo mwanzo nao kuwapangishia waliomo wao hawatawatambua na kuanzia mwezi ujao wataanza zoezi la kuingia mikataba mipya.


Aliwataka wapangaji hao kufuata maelekezo waliokubaliana kwenye kikao chao na wale walipangishia wengine watakuwa wamejiondoa wenyewe huku aliendani ndie wataingia nae mkataba mpya.


“Hiki kibanda no 46 tumekubaliana na mpangaji aliekuwepo ambaye tulimfungia kuendelea na biashara na huyo na mmliki wa awali sisi hatumtambui kwa teyari ameshajilipa mwenyewe”alisema Mollel.


Aidha akizungumzi eneo la Barcelona lenye eka mbili ambalo pia linamilikiwa na umoja huo alisema kuwa wametangaza zabuni za upangaji wa eneo hilo na atakayeshinda zabuni ndio ataendesha eneo hilo
.

Nae mwenyekiti wa umoja huo mkoani hapa Lengai ole Sabaya alisema kuwa suala la nyumba za umoja huo ambayo katibu aliekuwepo huko nyuma Kizigo alijiuzia kwa kiasi cha 3 milion kwenye eneo la Ngarenaro ataalipeleka ngazi za juu kwa maamuzi zaidi.


Wiki mbili zilizopita Uvccm mkoani hapa walitoa tamko lao mbele ya waandishi wa habari ambapo alikemea vikali mikataba iliyoingia ya upangishaji wa vibanda vya umoja huo na kujikuta wakiwa hawana kitu huku fedha zikichuliwa na wapangaji wao kwa mikataba minono ya 450,000 huku umoja huo ukiambulia 5000 kwa kibanda namba 46 haliiliyopekea kuingia na sera mpya ya mikataba ya vibanda hivyo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni