UPIGAJI KURA KATIKA UCHAGUZI MKUU ZAMBIA WAANZA HUKU KUKIWA NA ULINZI MKALI

Zoezi la upigaji kura za urais na ubunge limeanza nchini Zambia baada ya kumalizika kwa kampeni zilizokabiliwa na mapambano baina ya wafuasi wa vyama vinavyokinzana.

Uchaguzi huu unatarajiwa kuwa ni wa upinzani mkali baina ya rais Edgar Lungu wa chama cha PF na mgombea wa upinzani wa chama cha UPND, Hakainde Hichilema.

Kwa mara ya kwanza, mgombea wa urais nchini humo atalazimika kushinda kwa zaidi ya asilimia 50 ya kura zote, ili kuepuka uchaguzi wa marudio.
                        Rais Edger Lungu akihutubia katika moja ya mikutano ya kampeni
                             Mgombea urais wa chama cha upinzani Hakainde Hichilema

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni