Waziri
 wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akifafanua jambo katika 
mkutano na wachimbaji pamoja na watumiaji wa makaa ya mawe (hawapo 
pichani) uliojadili changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo. Mkutano 
huo ulifanyika Agosti 24, mwaka huu, Makao Makuu ya Wizara, jijini Dar 
es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini, Profesa 
James Mdoe.
 Naibu
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, 
Profesa James Mdoe, akizungumza na wachimbaji pamoja na watumiaji wa 
makaa ya mawe (hawapo pichani), wakati wa Mkutano baina yao na Waziri wa
 Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani).  Mkutano 
huo ulifanyika hivi karibuni, Makao Makuu ya Wizara hiyo jijini Dar es 
Salaam.
 Waziri
 wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) na Naibu 
Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe (kushoto kwa 
Waziri), wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa yakiendelea wakati wa 
Mkutano baina ya Wizara na wachimbaji pamoja na watumiaji wa makaa ya 
mawe, uliofanyika Agosti 24 wizarani, jijini Dar es Salaam.
Wajumbe
 mbalimbali walioshiriki Mkutano baina ya Waziri wa Nishati na Madini, 
Profesa Sospeter Muhongo na Wachimbaji pamoja na Watumiaji wa Makaa ya 
Mawe, wakifuatilia mijadala mbalimbali katika Mkutano huo uliofanyika 
Agosti 24 mwaka huu Makao Makuu ya Wizara jijini Dar es Salaam.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni