Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla amefanya ziara ya kikazi katika Zahanati na vituo vya
 Afya katika Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara ambapo ametoa maagizo 
mbalimbali yafanyiwe kazi huku suala la watumishi likibainika kuwa ni 
tatizo katika Wilaya hiyo.
Naibu
 Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla aliweza kutembelea Zahanati ya Hunyari 
iliyopo Kijiji cha Hunyari, Zahanati ya Kihumbu, Maliwanda, Kituo cha 
Afya Mugeta, Zahanati ya Sanzate, Kituo cha Afya Ikizu.
Aidha,
 amewataka watendaji na Halimshahuri hiyo kuhakikisha wanakamilisha 
maboresho na utekelezaji mwingine ikiwemo kwa Mganga Mkuu wa Wilaya 
kupanga safu ya ufanyaji wa kazi kwa kuwapeleka watalaamu katika 
Zahanati hizo ili kuwahudumia wananchi walio pembezoni.
Kwa
 upande wake, Mbunge wa Jimbo la Bunda Vijijini, Mh. Boniface alipongeza
 ziara hiyo kwani wameweza kubaini changamoto mbalimbali zinazoikabili 
sehemu ya utoaji wa huduma za Afya hivyo ujio wake huo kwenye maeneo 
hayo ya Vijijini yamewafungua macho.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akitembelea kukagua shughuli za ufanyaji kazi wa 
Zahanati ya Hunyari
Jengo maalum la wodi ya Wazazi la Zahanati ya Hunyari ambalo limejengwa kwa nguvu za wananchi.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akipatiwa maelezo kutoka Mkurugenzi wa Wilaya ya 
Bunda namna watakavyoisaidia Zahanati hiyo
Mbunge
 wa jimbo la Bunda Vijijini, Mh.Boniface Mwita Getere akimtambulisha 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. 
Dk. Hamisi Kigwangalla pamoja na viongozi wengine akiwemo Mkuu wa Wilaya
 ya Bunda Bi.Lydia Simeon Bupilipili.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akitoa maelezo na kupongeza wananchi wa kuweza 
kuchangia juhudi za ujenzi wa jengo la wodi la akinamama, Kulia ni Mkuu 
wa Wilaya ya Bunda Bi.Lydia Simeon Bupilipili.
Moja
 la jengo la Zahanati ya Kihumbu ambalo nalo mejengwa kwa nguvu ya 
wananchi kama linavyoonekana ambalo Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla aliweza 
kulitembelea kukagua ujenzi wake.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akitoa maagizo kwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bunda, 
Dk. Jonathan Ezekiel Budenu ( Wa tatu kulia) afanyie haraka marekebisho 
ya upungufu wa wafanyakazi hasa maeneo ya vijijini.
Mbunge
 wa jimbo la Bunda Vijijini, Mh.Boniface Mwita Getere akielezea jambo 
kwa wananchi wa Kijiji cha Mugeta wakati Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo
 ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla 
alipotembelea kituo hicho cha Mugeta.
Moja ya jengo la Zahanati ya Sanzate ambalo limejengwa kwa nguvu za wananchi kama linavyoonekana pichani.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akikagua jengo hilo la Sanzate ambalo limejengwa kwa 
nguvu za wananchi.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akitoa maagizo kwa watendaji wa kijiji cha Sanzate.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akiwasili kijiji cha Makongoro kukagua Kituo cha Afya
 Ikizu.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akiwaonyesha bomba linalotakiwa kuwekwa katika chumba
 cha upasuaji wakati wa kuingia kwenye chumba cha upasuaji.
msafara ukiendelea.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akipatiwa maelezo namna mashine kubwa ya kisasa ya 
ufuaji nguo ambayo ilitolewa na Wizara ya Afya ambayo hata hivyo Kituo 
hicho wameshindwa kuifanyia kazi.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akionyeshwa moja ya majokofu ya kuhifadhia mahiti 
kwenye kituo cha Afya Ikizu.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akikabidhi Wheel chair kwa ajili ya wagonjwa wa kituo
 cha Afya cha Ikizu ambapo Mbunge wa jimbo hilo, Mh. Boniface Getere 
alizitoa kama mchango wake.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akikabidhi Wheel chair kwa ajili ya wagonjwa wa kituo
 cha Afya cha Ikizu ambapo Mbunge wa jimbo hilo, Mh. Boniface Getere 
alizitoa kama mchango wake.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akiaga wakati alipotembelea kwa karakana ya uchongaji
 ambayo ina historia ndefu.
eneo la karakana ambayo ina historia ndefu ambapo jengo hilo ndipo palipochongwa kifimb cha Hayati Mwalimu Julius Nyerere.
Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. 
Hamisi Kigwangalla akiwa pamoja na viongozi wa Wilaya hiyo ya Bunda 
wakati wa kumaliza ziara hiyo ya kutembelea vituo vya Afya katika Wilaya
 ya Bunda.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni