VIVIAN CHERUIYOT WA KENYA ASHINDA MEDALI YA DHAHABU MBIO ZA MITA 5,000

Mwanariadha wa Kenya Vivian Cheruiyot ameshinda mbio za mita 5,000 na kumshinda Ayana Almaz wa Ethiopia ambaye alikuwa wakitarajiwa kushinda mbio hizo lakini akaishia kupata medali ya shaba.

Almaz, 24, alishinda mbio za mita 10,000 na kuweka rekodi wiki iliyopita na alitarajiwa kushinda pia mbio hizo za mita 5,000 ili kutwaa medali mbili za dhahabu katika michuano ya Olimpiki Jijini Rio.

Hata hivyo bingwa huyo wa dunia wa mbio za mita 5,000 alipitwa na Cheruiyot katika mita 2,000 pamoja na mwanariadha mwingine wa Kenya Hellen Onsando Obiri, aliyeshinda medali ya fedha.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni